• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AWAFUNDA MAAFISA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI WILAYANI HUMO

Posted on: August 23rd, 2023

Na Elinipa Lupembe

Maafisa watendaji wa kata na vijiji wilaya ya Arumeru inayojumuisha halmashauri mbili za Arusha na Meru, wamekutana na kukumbushana utekelezaji wa majukumu yao  unaozingatia kanuni, sheria na taratibu za utumishi wa Umma.


Maafisa hao wamepewa somo hilo na mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda kwa kushirikiana na Watalamu wa fani mbalimbali, wakati wa kikao kazi cha siku moja, chenye lengo la kuwajengea uwezo ili kuwa na uelewa wa pamoja juu ya usimamizi wa fedha na miradi ya maendeleo pamoja na kukumbushana utekelezaji wa majukumu yao, kikao ilichofanyika kwenye ukumbi wa shule ya  wa Fikiria Kwanza eneo la USA-River.

Mkuu huyo wa wilaya ameweka wazi kuwa lengo la kikao kazi hicho ni kuwajengea uwezo na uelewa wa pamoja usimamizi na utunzaji wa fedha za Umma, kujadili changamoto zinazowakabili pamoja na  kukumbushana utekelezaji wa majukumu yao kwa serikali na wanannchi.

Aidha ameeleza kuwa, kutokana muundo na lengo la Serikali kugatua madaraka kwa Serikali za Mitaa ni kusogeza huduma karibu na wananchi, hivyo Maafisa Watendaji, wanayo dhamana kubwa ya kuwajibika katika mnyororo mzima wa agenda ya kusukuma gurudumu ka maendeleo ya jamii na Taifa kwa  kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwenye maeneo yao, kupitia ofisi za kata na vijiji.

"Mtendaji wa kata na kijiji, Serikali imekupa dhamana kubwa ya kusimamia shughuli zake zote za serikali katika eneo lako,  tambueni kuwa majukumu makubwa ya serikali za mitaa yako mikononi mwenu, nyinyi ndio wasimamizi na watekelezaji wa shughuli zote za maendeleo ya nchi hii, hakikisheni mnafanya kazi kwa waeledi kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu zinazoelekezwa na serikali, tumieni hekima, busara na maarifa kutekeleza majukumu yenu". Amesisitiza Mhe. Emmanuela

Amewakumbusha majukumu yao ni usimamizi wa shuguli zote za serikali katika maeneo yao, ikiwa ni pamoja na usimamizi wa fedha zote za Umma katika maeneno yao, usimamizi wa miradi ya maendeleo, ulinzi wa amani, wasimamizi wa watalamu kweny maeneo yao.

Hata hivyo Mkuu huyo wa wilaya amekemea tabia ya baadhi ya watedaji, kutokuwa waaminifu katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa kufanya vitendo ambavo ni kinyume na maadili ya utumishi wa Umma, wapo wanaofanya ubadhilifu wa fedha za Umma, matumizi ya fedha yasiyozingatia taratibu, na baadhi yao kuungana na wenyeviti wa vijiji na wenyeji kuuza maeneo kwa njia zisizo halali jambo linalosababisha migogoro na wananchi kukosa haki zao na baadhi kutokuwa na imani na serikali yao.

"Baadhi ya watendaji mmekuwa sio waaminifu mmesababisha migogoro na kuwaacha wananchi kuwa na kero na malalamiko mengi kwa kuwanyima haki zao kwa maslahi yenu binafsi, ninawaasa mkiwa kama viongozi wekeni mbele maslahi ya Umma, fanyeni kazi kwa kuzingatia maadili ya uongozi, simamieni haki na wajibu wenu ili kila mwananchi wapate haki yake, msiwe chanzo cha migogoro kwenye maeneo yenu". Amesisitiza Mhe. Emmanuela

Awali kikao kazi hicho kilichobeba mada za Majukumu ya Watendaji wa kata na vijiji, matumizi ya mifumo ya malipo na ukusanyaji wa mapato ya fedha za Umma, taratibu za utoaji wa vibali vya ujenzi, jukumu la Watendaji katika  mapambano dhidi ya rushwa, Ushiriki wa Watendaji katika kuimalisha ulinzi na usalama katika maeneo yao.








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.