• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AWAJULIA HALI MAJERUHI WA AJILI HOSPITALI YA RUFAA MOUNT MERU....

Posted on: September 16th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda amewatembelea na kuwajulia hali majeruhi wa ajali ya gari kwaaliolazwa kwenye hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Arusha Mount Meru, iliyotokea tarehe 14.09.2023, eneo la Kisongo mkoani Arusha, iliyohuaisha gari aina ya Toyota Hiace.

Mhe. Emmanuela amefika hospitalini hapo ili kuwajulia hali majeruhi wa ajali pamoja na kuwapa pole ndugu jamaa na marafiki waliopoteza ndugu zao walifariki kwenye ajali hiyo, waliofika kwenye jengo la kuhifadhia maiti,  kubeba miili ya wapendwa  wao.

Aidha, amesema kuwa, Serikali imefanya juhudi kubwa katika suala la uokoaji wa maisha ya watanzania hao kupitia jeshi la polisi tangu ajali ilipotokea na kuhakikisha  afya za majeruhi wote zinaimarika bila kuwadai gharama zozote za matibabu hadi pale watakapo pata nafuu na kuendelea na majukumu yao ya ujenzi wa Taifa.

"Serikali imechukua jukumu la kugharamia gharama zote za matibabu kwa majeruhi wa ajali hiyo hadi pale afya zao zitakapoimarika na kurejea kwenye majukumu yao ya kawaida" Amesema.

Hata hivyo ametoa wito kwa madereva wote wa magari kuwa waangalifu wanapotumia vyombo vya moto kwa kuzingatia sheria zote za barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima, zinazotokea mara kwa mara na kugharimu maisha ya watanzania.

Naye Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha Mount Meru, Dkt. Alex Erinest amesema kuwa walipokea miili 6 na majeruhi 9, ambapo miili 5 imetambuliwa na ndugu zao na mwili mmoja bado haujatambulika.

Aidha, majeruhi 7 wamelazwa kwenye wodi huku majeruhi 2 wakiwa wamelazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi huku hali zao zikiendelea kuimarika kutokana na juhudi zinazoendelea kufanywa na jopo la madaktari wakishirikiana na wauguzi.

Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi ambao ndugu yao haonekani, kufika hospitalini hapo kwaajili ya kupata taarifa na kuutambua mwili huo ambao hadi sasa haujatambulika.


MATUKIO KATIKA PICHA


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.