Na Elinipa Lupembe.
Mwenyekiti wa kamati ya Sensa wilaya na Mkuu wa wilaya ya Arumeru, na Mhandisi Richard Ruyango, amewataka watendaji wa halmashauri ya Arusha, kushiriki kwa pamoja kuhakikisha wananchi wa halmashauri hiyo wanahesabiwa siki ya Sensa ya watu na makazi 23.08.2022 .
Mkuu huyo wa wilaya ameyasema hayo, wakati wa kikao kazi cha Sensa , kilichowakutanisha Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata na Vijiji pamoja wa halmashauri hiyo, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Arusha.
Hata hivyo Mhandisi Ruyango amewataka Maafisa hao kushirikiana na viongozi wote wa vyama na serikali, dini, mila na viongozi wa jumuia mbalimbali ndani ya wilaya ya Arumeru, katika maeneo yao kuhakikisha wanashiriki zoezi hili la Sensa ya watu na makazi kwa kuhamasisha watu wanaowaongoaza katika maeneo yao kuhesabiwa katika zoezi hilo la Sensa.
Aidha amezitaka kamati za Sensa za kata na vijiji kujikita katika kutoa taarifa zote za kijamii, zitakazohitajika kwenye dododso la Jamii kuwa wana uelewa wa kutosha wa eneo hilo pamoja na huduma zinazopatikana katika maeneo yao.
"Makarani wanapofanya kazi kwenye maeneo yetu, viongozi wote tuhakikishe taarifa zote za huduma za kijamii zinaingizwa kwenye dodoso la jamii ikiwemo taasisi zilizopo katika eneo yako, miundombinu ya majinna barabara, matukio mbalimbali kama majanga ya moto na njaa, hii inawahusu moja kwa moja viongozi" Amesisitiza Mkuu huyo wa wilaya
Akizungumza kwa niaba ya waheshimiwa madiwani, Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung'u Salekwa amebainisha kuwa tayayari wenyeviti wa Sensa ngazi ya kata ambao ni madiwani, wameanza kuhamasisha wananchi kushiriki zoezi hilo la Sensa katika maeneo yao na kuweka wazi kuwa wananchi wengi wana uelewa juu ya Sensa ya mwaka huu kutokana na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kuifanya kuwa shirikishi kwa kutumia majukwaa tofauti kuielezea Sensa.
Naye Mkurugenzi Mtendaji, halmasahuri ya Arusha, Seleman Msumi amesema kuwa yeye na watalamu wa halmashauri hiyo wamejipanga kuhakikisha zoezi la Sensa linafanyika kwa usahihi kwa kuhamasisha pamoja na kuhakikisha kila mkazi wa halmasahuri hiyo anahesabiwa na kama ilivyo malengo ya serikali.
Awali mkuu wa wilaya ya Arumeru, atakutana na viongozi wote wa wananchi na kijamii kimakundi ikiwemo, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa mila na dini.
SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI
JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.