• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AZITAKA NGO's KUTEKELEZA MIRADI KWA KUZINGATIA MAHITAJI YA JAMII HUSIKA..

Posted on: November 1st, 2022

Na Elinipa Lupembe

Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO's), halmashauri ya Arusha, yametakiwa kutekeleza miradi inayozingatia mahitaji ya jamii husika kwa kujikita katika kutekeleza vipaumbele vya serikali huku yakizingatia sheria na taratibu za uendeshaji wa mashirika nchini.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, wakati wa kikao cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli zilizofanywa na Mashirika hayo kwa kipindi cha robo ya kwanza, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.

Mkuu huyo wa wilaya licha ya kuridhishwa na taarifa za utekelezaji zilizowasilishwa na mashirika hayo, ameyasisitiza mashirika hayo, kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi na vipaumbele vya serikali kisekta.

"Nimeridhishwa na kazi zinazofanyika, kwa kuwa zimejikita kutatua changamoto za jamii kwenye sekta ya elimu, afya, kilimo, lishe, biashara na ujasiriamali, uhifadhi na utunzaji wa mazingira, kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto, lakini zaidi napongeza suala la kupambana na mmea hatari wa gugu karoti". Amebainisha Mhandisi Ruyango.

Aidha ameyaagiza mashirika hayo kuandaa mikakati ya kuanza  kutoa elimu kwa makundi ya viongozi ili kuwajengea uwezo wa kuwa na maadili ya uongozi ili kuwa na viongozi wanaozingatia mustakabali mzima wa utawala bora kwa jamii.

Hata hivyo Mkuu huyo wa wilaya ameweka wazi kuwa, serikali inatambua na kuthamini kazi zinazofanywa na mashirika hayo, ikiwa ni utekelezaji wa malengo ya serikali ya kuwahudumia wananchi, kazi ambazo zilipaswa kufanywa na serikali.

Nao wawakilishi wa mashirika hayo wameishukuru serikali kwa kuyaamini mashirika na kushirikiana nayo katika kutoa huduma za jamii kwa niaba ya serikali zaidi wakimpongeza mheshimwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutambua na kuthamini kazi zinazofanywa na ASAS za kiraia huku akiisisitiza serikali kuweka mazingira wezeshi kwa mashirika.

Herieth Raju mwakikishi wa shirika la GLAMI ameishukuru halmashauri kwa ushirikiano na amewataka wadau wanaofanya kazi zinazofanana, kushirikiana na kufanyakazi kama timu pamoja na kubadilishana uzoefu kwa kuweka mikakati ya kuhudumia jamii kwa pamoja ikiwa ni kuhamasisha na kuwajengea  wananchi uwezo wa kujitegemea.

"Kwa mfano Mashirika yanayosupport wanafunzi kupata chakula shuleni, wawajengee uwezo wazazi wa kutambua kuchangia chakula cha watoto wao shuleni ni jukumu lao, badala ya kuwapa chakula cha bure kwa miaka yote, jambo linalowafanya baadhi ya wazazi kubweteka na kuona kama hilo si jukumu lao". Amesema Herieth

Naye Msajili wa Mashirika halmashauri ya Arusha Ahadi Mlay, ameyapongeza mashirika hayo kwa ushirikiano sambamba na uwasilishaji wa taarifa za robo kwa wakati na kuwasisitiza, kuhakikisha wanatekeleza shughuli zao kama maandiko ya miradi yao yanavyoelekeza na si vinginevyo.

Awali kikao hicho ni kikao cha robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kipindi cha Julai - Septemba 2022 ni cha kawaida kwa mujibu wa kanuni na miongozo ya serikali za mitaa, inayoyataka mashirika yasiyo ya kiserikali, kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli zinazofanyika kwa kila robo ya mwaka huku jumla ya mashirika 30 kati ya 38 yamewasilisha taarifa zake.


ARUSHA DC

KaziInaendelea ✍✍✍.











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.