Na Elinipa Lupembe
Uongozi wa halmashauri ya Arusha, umemshukuru mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan na Serikali ya awamu ya sita kwa kutoa pikipiki kwa ajili ya ufuatiliaji wa masuala ya Lishe hususani watoto wenye utapiamlo.
Akizunguza wakati wa kukabidhi pikipiki hizo kwa watalamu wa Idara ya Afya, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amemshukuru mheshimiwa Rais kwa mgao huo wa pikipiki, vitendea kazi ambavyo vitarahisisha ufuatiliaji wa watoto wanaokabiliwa na changamoto ya utapiamlo.
"Tunamshukuru Mama Samia, tumegawa pikipiki hizi kwenye maeneo ambayo yana idadi kubwa ya watoto wenye utapiamlo, licha ya kwamba zitawasaidia watalamu wetu lakini zitarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wepesi kwa watoto wenye utapiamlo". Amesisitiza Mkurugenzi huyo.
Afisa Lishe halmashauri ya Arusha, Doto Milembe, amethibitisha kuwa, mgao wa pikipii hizo umezingatia maeneo yenye idadi kubwa ya watoto wenye utapiamlo mkali kwa lengo la kuwarahisishia watalamu kufanya ufuatiliaji kwa watoto waliopatiwa matibabu kwa kushirikiana na wahudumu ngazi ya jamii.
"Pikipiki hizo zitakuwa msaada mkubwa kwa watalmu kuweza kuwafikia watoto kwenye kaya, kufanya ukaguzi wa vyakula pamoja na upimaji wa madini joto kwenye chumvi shuleni na madukani, pamoja na kufanya kufanya tathmini ya kwenye kaya". Amefafanua Doto
Hata hivyo watalamu waliokabidhiwa pikipiki hizo, wameishukuru serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na Mama Samia Suluhu Hassan kwa kutoa vitendea kazi hivyo, vitakavyorahisisha utekelezaji wa majukumu yao kwa jamii.
Nuru Ally, Muuguzi wa zahanati ya Nameloki, kijiji cha Losinoni Juu, ameweka wazi kuwa, licha ya pikipiki hiyo kumrahisishia usafiri wa kuwafikia watoto, itaongeza tija na ufanisi katika kazi ya kuwahudumia watoto wenye utapiamlo pamoja na kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa lishe bora kwa watoto.
"Hiki ni kitendea kazi cha muhimu kutokana na changamoto ya ugumu wa kufikika kwa baadhi ya maeneo katika kata ya Musa, pikipiki itaniwezesha kuwafika na kuwahudumia watoto wengi kwa muda mfupi, tofauti na hapo awali". Amesisitiza Lugito Nzala Muuguzi Zahanati ya Musa
Ifahamike kuwa serikali imetoa pikipiki kwa halmashauri zote nchini kwa ajili ya ufuatiliaji wa masuala ya Lishe, hususani kwa watoto wenye utapiamlo mkali, huku halmashauri ya Arusha ikiwa ni miongozi mwao kwa kuoata jumla ya pikipiki tatu.
ARUSHA DC
KaziInaendelea ✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.