• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DED ARUSHA DC AITAKA JAMII KUSAIDIA WATOTO WENYE UHITAJI

Posted on: February 8th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi ameitaka jamii, kuhudumia watoto wenye uhitaji katika maeneo yao, kwa kufanya hivyo kunawapa watoto hao faraja na zaidi inasaidia watoto hao kufikia malengo na ndoto zao.

Mkurugenzi Msumi ameyasema hayo ofisini kwake, wakati akiwakabidhi msaada watoto wenye uhitaji, kata ya Kiutu, msaada ambao umewezeshwa na halmashauri kwa kushirikinana na wasamaria wema pamoja na wadau wa maendeleo halmashauri ya Arusha.

Msumi amesisitiza kuwa, licha ya serikali kuwa na mpango na mikakati ya kusaidia watoto hao, kupitia programu ya mpango wa kunusuru kaya masikini lakini bado haijaweza kufanikiwa kuwafikia watoto wote,  kulingana na idadi kubwa ya watoto wenye uhitaji nchini, na kuongeza kuwa jamii inahitajika kujitoa kwa hali na mali, kusaidia watoto hao, ndani ya jamii zao.

"Tunawafahamu watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, watoto wenye uhitaji tunaishi nao, niwasihi  wanajamii kujitoa kusaidia watoto wenye hao kwenye maeneo yetu, jambo ambalo linasisitizwa hata kwenye imani za dini zetu , kiimani wanasema, 'nyumba inayohudumia watoto wenye uhitaji inawaka taa mbele za Mungu' na 'nyumba isiyohudumia wenye uhitaji, taa imezimika' tuwe taa inayowaka ni baraka mbele za Mungu pia" amesisitiza Mkurugenzi huyo.

Aidha Mkurugenzi Msumi amewashukuru wadau na wasamaria wema waliojitoa, kutoa msaada huo kwa watoto wenye uhitaji, na kuwataka wadau wengine kujitokeza kusaidia watoto hao, kwani hilo ni jukumu la wanajamii wote. 

Afisa Ustawi wa Jamii, Halmasahuri ya Arusha, Beatrice Tengi, amesema kuwa, halmashauri kwa kushirikiana na shirika la Huruma Ophanage na msamaria mwema, wametoa msaada wa vyakula, sabuni, madaftari na kalamu kwa watoto 50 wa kata za Kiutu, Mwandeti, Bwawani, Bangata na Oljoro.

Amefafanua kuwa  watoto hao 50 wamegawiwa mchele Kilo 5, maharage Kilo 3, sabuni ya unga mche 1, na pakiti 1 ya sabuni ya unga, madaftari 4 na kalamu kwa kila mmoja na baadhi yao wamepatiwa nguo kulingana na uhitaji.

Halmashauri ya Arusha inawakaribisha wadau wa maendleeo na wasamaria wema, kuendelea kujitoa kwa hali na mali kutoa msaads kwa watoto wahitaji, walio kwenye vituo maalumu na wale wanaoishi ndani ya jamii.

ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍✍✍

PICHA ZA 







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.