Na. Elinipa Lupembe
Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amezindua rasmi ujenzi wa kituo kipya cha Afya cha Oloirieni, kinachojengwa katika kata ya Oloirieni, mradi unaotekelelezwa na halmashauri kupitia fedha za fidia ya deni la Lakilaki, mradi utakaogharimu kiasi cha shilingi milioni 450.
Katika uzinduzi huo, mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, amefanya ishara ya kuanzisha uchimbaji wa msingi wa majengo matatu ya kituo kituo hicho kipya cha afya, tukio lililoshuhudiwa na wakazi wa kitongoji cha Oloirieni, wajumbe wa kamati ya ujenzi wa kituo hicho cha afya, watalamu wa ngazi ya kata na ngazi ya halmashauri ikijumuiasha Wakuu wa Idara na Vitengo, zoezi lililofanyika kwenye kitongoji cha Oloirien ambapo mradi huo umeanza kutekelezwa.
Mkurugenzi Msumi, amewataka wananchi wa Oloirieni kutambua kuwa mradi huo ni mali yao, hivyo wanajukumu kubwa la kushiriki katika usimamizi wa mradi huo katika hatua zote za ujenzi kama taratibu za forced akaunti unavyoelekeza, pamoja na kuhakikisha ulinzi wa vifaa vyote vinavyoletwa katika eneo hilo la ujenzi huku akwataka wajumbe wa kamati ya ujenzi kuhakikisha wanasimamia vema hatua zote za utekelezaji wa mradi huo.
"Kamati ya ujenzi, mmepewa dhamana na wananchi wenzenu ya kusimamia ujenzi wa kituo chao cha afya, hakikisheni mnasimamia kwa kufuata taratibu zote za ujenzi, kama zinavyoelekezwa na serikali, ili muweze kupata majengo yenye ubora kulingana na thamani ya pesa, tambueni fedha hizo ni kodi za wananchi, kuweni wazalendo katika usimamizi wa mradi huu utakaotumia fedha nyingi za umma" amesisitiza Mkurugenzi Msumi.
Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimwa Rais, mama Samia Suluhu Hassan, inawajali wananchi wake, kwa kutekeleza mkakati wake wa kuhakikisha kila kata inakuwa na kituo cha afya chenye hadhi ya nyota tano, lengo kubwa likiwa ni kusogeza huduma za afya karibu na wananchi pamoja na kutokomeza vifo vya kina mama na watoto wakati wa kujifungua.
Naye Afisa Mipango, halmashauri ya Arusha, Anna Urio amebainisha kuwa kiasi hicho cha shilingi milioni 450 kitatumika kujenga majengo matatu ikiwemo jengo la wagonjwa wa nje 'OPD', jengo la mama na mtoto 'martenity word', jengo la maabara, kichomea taka 'incinerator' na kusisitiza kuwa mradi huo unategemea kukamilika mwishoni mwa mwaka huu wa 2021.
Hata hivyo wananchi wa kata ya Oloirieni wameishukuru serikali kwa kuwakumbuka na kuwajengea kituo cha afya, jambo ambalo lilikuwa ni ndoto katika kata hiyo, na kuthibitisha kuwa, uwepo wa kituo hicho cha afya, utawewezesha kupata huduma bora za afya ndani ya eneo la kata yao, jambo ambalo litawapunguzia gharama za usafiri na gharama za matibabu, tofauti na hapo awali walikwenda kutibiwa katika hospitali ya wilaya ya olturumeti ama Seliani Ngaramtoni ambayo ni hospitali ya kulipa.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Oloirieni mheshimiwa John Aminiel, amepongeza juhudi za serikali ya kuweka kipaumbele katika uboreshaji wa miundo mbinu ya afya nchini, huku utekelezaji wa Ilani ya CCM ya kuhakikisha kila kata inakuwa na kituo cha afya chenye hadhi ya nyota tano.
Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi, Ismail Marunda licha ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuwapatia mradi wa kituo cha afya katika kata yao, mradi ambao ameutaja kuwa ni wa muhimu sana kwa wakazi wa kata ya Oloirieni na majrani zao, na kuahidi kusimamia vema hatua zote za utekelezaji wa ujenzi wa kituo hiko ili kufikia malengo ya serikali ya kuwa na kituo bora cha afya.
Naye Sesilia Vanica, mwenyekiti wa kamati ya mapokezi ameweka wazi kuwa uwepo wa kituo cha afya katika kata ya Oloirieni utawanufaisha sana wanawake wa eneo hilo, kwa kuwa wananwake ndio waathirika wakubwa wa huduma za afya kwa familia zao na kuongeza kuwa kituo hicho kitapunguza vifo visivyo vya lazima hasa kwa wanawake wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano.
"Kwa sasa inatulazimu kwenda kutibiwa hospitali ya serikalia ya Olturumeti, hospitali ambayo iko mbali sana kutoka hapa, licha ya kuwa hapa jirani kuna hospitali ya binafsi kitu ambacho wananchi wengi hushindwa kwenda kwenye hospitali hiyo kwa kuwa hawana uwezo wa kifedha kugharamia matibabu, lakini uwepo wa kituo hicha cha serikali, kitaokoa maisha ya watu wengi hata wasio na uwezo kifedha" Amesisitiza Selilia.
Baaada ya kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho cha Afya, inakadiriwa kuhudumia takribani wagonjwa elfu 14 wa kata ya Oloirieni na vitongoji vyake pamoja na vitongoji vingine vya kata jirani.
MATUKIO KATIKA PICHA
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, akichimba msingi kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo kipya cha afya cha Oloirieni, mradi unaotekelezwa na fedha za Lakilaki kwa gharama ya shilingi milioni 450.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Oloirien, wakati wa uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo kipya cha afya cha Oloirieni, mradi unaotekelezwa na fedha za Lakilaki kwa gharama ya shilingi milioni 450.
Afisa Mipango, halmashauri ya Arusha Anna Urio, akichimba msingi kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo kipya cha afya cha Oloirieni, mradi unaotekelezwa na fedha za Lakilaki kwa gharama ya shilingi milioni 450.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Oloirieni mheshimiwa John Aminiel, akichimba msingi kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo kipya cha afya cha Oloirieni, mradi unaotekelezwa na fedha za Lakilaki kwa gharama ya shilingi milioni 450.
Afisa Elimu Msingi, halmashauri ya Arusha, mwalimu Hossein Mghewa, akichimba msingi kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo kipya cha afya cha Oloirieni, mradi unaotekelezwa na fedha za Lakilaki kwa gharama ya shilingi milioni 450.
Wananchi wa kata ya Oloirini waliojitokeza kwenye uzinduzi, mradi wa ujenzi wa Kituo kipya cha afya cha Oloirieni, mradi unaotekelezwa na fedha za Lakilaki kwa gharama ya shilingi milioni 450.
MICHORO YA MAJENGO YA KITUO KIPYA CHA AFYA CHA OLOIRIENI
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.