• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DED MSUMI AZINDUA UJENZI WA KITUO CHA AFYA OLOIRIENI - ARUSHA DC

Posted on: October 6th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amezindua rasmi ujenzi wa kituo kipya  cha Afya cha Oloirieni, kinachojengwa katika kata ya Oloirieni, mradi unaotekelelezwa na halmashauri kupitia fedha za fidia ya deni la Lakilaki, mradi uatakaogharimu kiasi cha shilingi milioni 450.

Katika uzinduzi huo, mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, amefanya ishara ya kuanzisha uchimbaji wa msingi wa majengo matatu  ya kituo kituo hicho cha afya, tukio lililoshuhudiwa na wakazi wa kitongoji cha Oloirieni, wajumbe wa kamati ya ujenzi wa kituo hicho cha afya, watalamu wa ngazi ya kata pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo, zoezi lililofanyika kwenye kitongoji cha Oloirien ambapo mradi huo unatekelezwa.

Mkurugenzi Msumi, amewataka wananchi wa Oloirieni kutambua kuwa mradi huo ni mali yao, hivyo wanajukumu kubwa la kushiriki katika hatua zote za utekelezaji wa mradi huo, ikiwemo usimamizi wa mradi huo katika hatua zote kama taratibu za forced akaunti unavyoelekeza, pamoja na kuhakikisha ulinzi wa vifaa vyote vinavyoletwa katika eneo hilo la ujenzi huku akwataka wajumbe wa kamati ya ujenzi kuhakikisha wanasimamia vema hatua zote za utekelezaji wa mradi huo.

"Kamati ya ujenzi, mmepewa dhamana na wananchi wenzenu ya kusimamia ujenzi wa kituo chao cha afya, hakikisheni mnasimamia kwa kufuata taratibu zote za ujenzi, kama zinavyoelekezwa na serikali, ili muweze kupata majengo yenye ubora kulingana na thamani ya pesa, tambueni fedha hizo ni kodi za wananchi, kuweni wazalendo katika usimamizi wa mradi huu wenye fedha nyingi za umma" amesisitiza Mkurugenzi Msumi.

Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimwa Rais, mama Samia Suluhu Hassan, inawajali wananchi kwa kutekeleza mkakati wake wa kuhakikisha kila kata inakuwa na kituo cha afya chenye hadhi ya nyota tano, lengo kubwa  ikiwa ni kusogeza huduma za afya karibu na wananchi pamoja na kutokomeza vifo vya kina mama na watoto wakati wa kujifungua.

Naye Afisa Mipango, halmashauri ya Arusha, Anna Urio amebainisha kuwa kiasi hicho cha shilingi milioni 450 kitatumika kujenga majengo matatu ikiwemo jengo la wagonjwa wa nje 'OPD', jengo la mama na mtoto 'martenity word', jengo la maabara, kichomea taka 'incinerator' na kuongeza kuwa maradi huo unategemea kukamilika mwisho mwa mwaka huu wa 2021.

Hata hivyo wananchi wa kata ya Oloirieni wameishukuru serikali kwa kuwakumbuka na kuwajengea kituo cha afya, jambo ambalo lilikuwa ni ndoto katika kata hiyo, na kuthibitisha kuwa, uwepo wa kituo hicho cha afya, utawewezesha kupata huduma bora za afya ndani ya eneo la kata yao, jambo amabalo litawapunguzia gharama za usafiri, tofauti na hapo awali walikwenda kutibiwa katika hospitali ya wilaya ya olturumeti ama Seliani Ngaramtoni.

Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi, Ismail Marunda licha ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuwapatia mradi wa kituo cha afya katika kata yao, mradi ambao ameutaja kuwa ni wa muhimu sana kwa wakazi wa kata ya Oloirieni na majrani zao .

Naye mwenyekiti wa kamati ya mapokezi Sesilia Vanica, ameweka wazi kuwa uwepo wa kituo cha afya katika kata ya Oloirieni utawanufaisha sana  wanawake wa eneo hilo, kwa kuwa wananwake ndio waathirika wakubwa wa afya za familia zao na kuongeza kuwa kituo hicho kitapunguza vifo visivyo vya lazima hasa kwa wanawake wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano.

"Kwa sasa inatulazimu kwenda kutibiwa hospitali ya serikali ya Olturumeti, hospitali ambayo iko mbali sana kutoka hapa, licha ya kuwa hapa jirani kuna hospitali ya binafsi kitu ambacho wananchi wengi hushindwa kwenda kwenye hospitali hiyo kwa kuwa hawana uwezo wa kifedha kugharamia matibabu, lakini uwepo wa kituo hicha cha serikali, kitaokoa maisha ya watu wengi hata wasio na uwezo kifedha" Amesisitiza Selilia.



Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akichimba msingi, kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha Afya Oloirieni kata ya Oloirieni.




Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akizungumza na wananchi wa kata ya Oloirieni mara baada ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha Afya Oloirieni kata ya Oloirieni.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Oloirieni, Mheshimiwa ...... akichimba msingi, kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha Afya Oloirieni kata ya Oloirieni.


Afisa Mipango Halmashauri ya Arusha, Anna Urio, akichimba msingi, kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha Afya Oloirieni kata ya Oloirieni.


Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Arusha, mwalimu Hossein Mghewa, akichimba msingi, kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha Afya Oloirieni kata ya Oloirieni.


Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa kituo cha Afya Oloirieni  Ismail Marunda, akichimba msingi ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa maradi wa ujenzi wa Kituo Kipya cha Afya cha Oloirieni.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA August 14, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA BW. SELEMAN MSUMI AWASHONEA SARE MADEREVA WA HALMASHAURI HIYO

    October 02, 2025
  • WIZARA YA KILIMO KUPITIA MAMLAKA YA UDHIBITI WA NAFAKA NA MAZAO MCHANGANYIKO (COPRA) YAZINDUA RASMI MSIMU WA UNUNUZI WA ZAO LA PARACHICHI KWA MWAKA 2025/2026

    September 27, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ARUMERU MWINYI AHMED MWINYI AHITIMISHA MAFUNZO YA JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT)

    September 21, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA AWAASA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA USAFI

    September 21, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.