• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DSW NA KITUO SALAMA CHA WASICHANA KIJIJI CHA IMBIBYA

Posted on: October 1st, 2022

Na Elinipa Lupembe

Katika kuimarisha harakati za kupinga ukatili kwa wasichana, Shirika la DSW limejenga Kituo Salama cha Wasichana kijiji cha Imbibya kata ya Mwandet, halmashauri ya Arusha lengo likiwa ni kuwapa eneo wasichana la kuweza kukaa na kubadilishana uzoefu, kujifunza stadi za maisha katika kasuala mbalimbali ya vijana.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo hicho, mkurugenzi wa shirika la DSW, Peter Owaga, amesema kuwa, kupitia mradi wa Binti na Maendeleo (BIMA), shirika limekuwa likifanya shughuli mbalimbali na wasichana, na hatimaye kuamua kuwajengea eneo la kudumu la kukutania na kupata mafunzo kwa uhuru, utulivu na kwa mapana zaidi.

Jengo hili litatumika kama darasa na maktaba ya kutoa mafunzo kwa wasichana na vijana, ambapo wasichana wa rika balehe watakutanishwa na watalamu wa kada tofauti na kuwapa elimu ya stadi za maisha, kujitambua na kukabiliana na ukatili wa kijinsia, Afya ya uzazi kwa vijana, uongozi, ujasiriamali na namna ya kujikwamua kiuchumi.

"Kituo kitawapa fursa vijana ya kukaa pamoja na kubadilishana uzoefu masuala ya ujana na ukatili, lakini zaidi kuwakutanisha na watalamu watakaowaelimisha namna ya kukabiliana na changamoto za ujana ikiwemo ukatili na elimu ya ujasiriamali" . Amefafanua Mkurugenzi Mbego.

Naye mgeni rasmi na Afisa Maendeleo Mkoa wa Arusha, Erena Materu, licha ya kulishukuru shirika hilo kwa kushiriki kutekeleza malengo ya Serikali kwa kuwekeza nguvu zaidi kwenye vipaumbele vyake, na kuwataka wananchi wa Imbibya hususani vijana kutumia kituo hicho ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

"Vijana wa Imbibya mna bahati san, halmashauri ina vijiji vingi lakini kituo kimejengwa kwenu, kazi kwenu kutumia kituo hicho na watalamu watakao kuwepo, mkikitumia vizuri na kuleta matokeo mazuri, na vijiji vingine vitajengewa vituo hivi, tunawategemea mkawe mfano wa vijana wa 'Arusha DC' na mkoa mzima wa Arusha." Amebainisha Erena

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha,  Afisa Maendeleo ya Jamii - Dawati la Jinsia, Rovil Nguyaine, ameahidi kukisimamia kituo hicho kiweze kuwa endelevu hata pale mradi wa shirika utakapofika mwisho kwa kuhakikisha watalamu wanafika kituoni hapo kutoa huduma huku akiwasisitiza vijana kuhakikisha wanatumia kituo hicho ipasavyo.

Hata hivyo wananchi wa kijiji hicho, wamelishukuru shirika na halmashauri kwa kuhakikisha wanajenga kituo hicho, huku wakithibitisha, kupitia mradi wa Binti na Maendeleo, jamii imeanza kupata uelewa wa madhara ya ukatili wa kijinsia na kuanza kuachana na mila na desturi potofu.

"Kupitia mradi wa Binti na Maendeleo, jamii ya Imbibya imeanza kubadilika, kwa sasa ndoa za utotoni zimepungua, wasichana tunaendelea na masomo, hali ya ukeketaji imeanza kupungua licha ya kuwa bado kuna baadhi ya watu wanafanya kwa siri ila taratibu itafika mwisho" Amefafanua Glory Eliaman, mnufaika wa mradi wa BIMA

Awali DSW imetekeleza mradi wa Binti na Maendeleo kuanzia mwaka 2019 na utakamilika mwishoni mwa mwaka huu 2022, na kufanikiwa kujenga vituo salama kwa wasichana 2 na kuwafikia vijana 4,560, huku wadau 197 wakinufaika kupata elimu kwa ajili ya kwenda  kuelimisha na kuhamasisha jamii kupinga ukatili wa kijinsia katika maeneo yao.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA UZINDUZI WA KITUO SALAMA CHA WASICHANA















Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.