Kinababa sita wa Kamati ya Kutetea na Kupinga ukatili wa kingono na ulawiti kwa watoto wa kiume, halmashauri ya Arusha 'Father on Duty' wakiwa kwenye mdahalo na wanafunzi wavulana wa maabara ya kupinga ukatili wa kingono dhidi yao (Boy's Vac Lab), shule ya Msingi Naurei.
Kina baba hao, wamekutana na klabu ya watoto wavulana na kufanya mdahalo uliambatana na utoaji wa elimu kwa watoto hao juu ukatili wa kingono husani ulawiti kwa watoto wa kiume.
Mwenyekiti wa Kamati ya 'Father on Duty' Fanuel Sirikwa, ameelezea namna ya matukio ulawiti kwa wavulana yalivyoongezeka kwa kasi na kuwataka watoto kujitambua na kuchukua hatua ya kupinga vitendo hivyo kwa nguvu kubwa.
Aidha amewataka watoto hao, kupinga vitendo hivyo na kutoa taatifa kwa siri endapo watakutana na mtu atakayewashawishi kufanya hivyo ama endapo kuna mtoto au watoto wanafanya vitendo hivyo ili waweze kusaidiwa na kuachana na tabia hizo mbaya.
Hata hivyo wavulana hao wamekiri kufahamu tabia hizo na kuwa zinaendelea kwenye jamii yao, na kuwaomba wazazi na jamii, kuwasimamia watoto wao ili kuwaepusha na madhila hayo mabaya kwa watoto na taifa kwa ujumla.
Nasiri Shaban mwanafunzi wa darasa la VI shule ya Msingi Naurei, amewataka watoto kupinga vitendo hivyo haramu, kwa kuepuka vishawishi vya kuoewa zawadi ndogondogo, na kuimba jamii kuendelea kutoa elimu kwa watoto juu ya madhara ya ulawiti kiafya, kiakili na kijamii.
Halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na shirika la CWCD, linatekeleza mradi wa kupinga ukatili wa kingono na ulawiti kwa watoto wa kiume, kwa kuanzisha maabara za wavulana 'Boy's Vac Lab' katika shule sita za msingi za Naurei, Moivo, Ilboru, Olturoto, Kiranyi na Ngaramtono kwa ufathili wa Foundation for Civil Society.
TUPINGE UKATILI KWA WATOTO,
WATOTO NI TAIFA LA KESHO
UKIMLINDA ATAJENGA NCHI BAADAYE✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.