• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Arusha DC inatarajia kupokea Msaada wa magari matano kutoka Ujerumani

Posted on: October 5th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Arusha inategemea kupokea msaada wa magari matano kutoka kwa Kikundi cha 'Friend of German' la nchini Ujerumani  kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la Help for Maasai Children la nchini Tanzania mapema mwishoni mwa mwezi huu wa Oktoba.

Akizungumza kwa njia ya simu, Mratibu wa Mradi wa shirika hilo ndugu Harld Ppeiffer , ameyataja magari hayo kuwa ni pamoja na magari mawili ya kisasa kwa ajili ya huduma za haraka kwa wagonjwa wa dharura 'Ambulance'  na magari matatu aina ya Nissani kwa ajili ya kurahisisha usafiri kwa watalamu kufika kwenye maeneo ya wananchi wakati wa kutoa huduma.

Hata hivyo katika hali ya kipekee zaidi, Ppeiffer amesema kuwa, Shirika hilo limeamua kuleta magari hayo, kwa kuyaendesha kutoka nchini Ujerumani mpaka nchini  Tanzania, hususani kwenye ardhi ya Halmashauri ya Arusha huku safari yao ikiwa tayari  imeanza tangu tarehe 23.09.2028 na kutarajiwa kukamilika tarehe 17.10.2018.

Amefafanua kuwa, kupitia safari hiyo ya kuleta magari hayo, itakayochukua takribani siku kumi na nne, wadau hao wanategemea kukusanya fedha kiasi cha 'Euro 300,000, fedha ambazo zitakazotumika kwenye ujenzi wa Zahanati ya Oldonyowas iliyopo kata ya Oldonyowas na kiasi kingine kutumika katika shughuli nyingine za Idara ya Afya.

Naye Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Dkt, Wilson Mahera, amethibitisha ujio wa magari hayo kutoka shirika hilo na kusema kuwa, licha ya kulishukuru shirika hilo na serikali ya Ujerumani lakini pia magari hayo yamekuja wakati muafaka kwa kuwa halmashauri ilikuwa inakabiliwa na upungufu wa magari, ulikuwa kwa namna moja au nyingine ulikwamisha utekelezaji wa majukumu kiutendaji.

Amefafanua kuwa, magari manne kati ya hayo matano yatakabidhiwa kwa halmashauri ikiwa ni Nissan mbili  na Ambulance mbili, magari yatakayotumika na Idara ya Afya kwa kutoa huduma za afya kwa wananchi huku gari moja aina ya Nissan litatumiwa na shirika hilo la Help fo Maasai Children kwa ajili ya kusimamia hiyo miradi wanayoitekeleza ndani ya  Halmashauri.

Awali halmashauri ya Arusha imekuwa na uhusiano wa kirafiki na marafiki hao waishio Ujerumani,uhusiano ambao umeleta mafanikio makubwa ambayo, marafiki hao kuamua kuwasaidia wananchi wa Halmashauri hiyo  kwenye sekta ya Elimu, Afya na Maji kwa kupitia shirika la 'Help for Masaai Children'.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.