• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Hatimaye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Arusha DC apatikana

Posted on: October 29th, 2018

Kufuatia agizo la serikali la kuunda mabaraza ya wazee katika halmashuri zote, halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru imetekeleza agizo hilo kwa kukamilisha mchakato wa kuunda mabaraza hayo  na hatimye kumpata mwenyekiti wa Baraza la wazee ngazi ya Halmashuri, katika uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Viongozi wa Baraza la wazee kutoka kwenye kata zote, zinazounda Halmashauri ya Arusha Wilayani Arumeru, wamefanya uchaguzi wa viongozi watakaounda baraza hilo, katika ngazi ya Wilaya pamoja na wajumbe watakao wawakilisha katika baraza la Madiwani.

Akizungumza wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Kaimu Mwanasheria wa Halmashauri hiyo, Eliasifiwe Kileo, amemtangaza ndugu Elias Ngungat wa kata ya Olmotony, kuwa Mwenyekiti wa Baraza la wazee katika halmashuri ya Arusha, baada ya kupata kura 18 kati ya kura 50 zilizopigwa na kuwashinda wapinzani wake wanne waliogombea nafasi hiyo na kugawana kura 32 zilizosalia.

Aidha Kaimu Mwanasheria huyo, amewatangaza viongozi wengine watakaongoza baraza hilio ni pamoja na ndugu Aloyce Mollel kuwa Makamu Mwenyekiti, Julius Maras kuwa Katibu, na Florah Mollel kuwa Katibu msaidizi na mtunza Fedha ndugu Emaculata Lwali,  baada ya wote hao kuchaguliwa na kushinda kwenye uchaguzi huo.

Aidha Eliasifiwe amewataja wajumbe wawili wawakilishi ‘ME’ na ‘KE’ ambaye ni ndugu Yohana Mengarana na Rose Laizer, watakaowawakilisha Baraza la Wazee wa Halmashauri hiyo kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani pamoja na kwenye mkutano wa Kamati ya kudumu ya UKIMWI.

Awali kabla ya uchaguzi huo kufanyika, Afisa Ustawi wa Jamii kitengo cha Wazee na Walemavu, Beatrice Tengi aliwaelezea Wazee hao, lengo uchaguzi huo ni kupata viongozi, watakao wawakilisha wazee wenzao kwenye ngazi ya wilaya, mkoa na hatimaye taifa.

Aidha Beatrice aliwataka wazee kuwachagua viongozi makini, watakaoweza kuwasilisha kero zao pamoja na kutetea maslai ya wazee ili kuhakikisha kila mzee anapata haki sawa kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza baada ya uchaguzi huo, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Arusha, Mganga Mkuu wa halmashauri Dkt. Peter Mboya, licha ya kuwapongeza viongozi waliochagulia, amewataka kuwawakilisha vema wazee wenzao waliowaamini na kuwapa dhamana kwa kuzitendea haki nafasi walizopewa ipasavyo pamoja na kuhakikisha wazee wanapata haki zao za msingi.

“ Ushindi mlioupata ni dhamana, mnatakiwa kuitendea haki nafasi hizo, kwa kuwatetea wazee wenzenu kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya kimaendeleo na ustawi wa wazee wa taifa hili, tekelezeni majukumu yenu ipasavyo kwa namna mtakavyoelekezwa na kitengo cha Ustawi ya Jamii ” amesisitiza Dkt. Mboya

Daktari Mboya, amewathibitishia wazee hao kuwa, halmashauri ya Arusha, imeandaa mikakati mbalimbali ya kuboresha huduma za wazee ikiwemo huduma muhimu ya afya kwa kuweka madirisha maalumu ya matibabu kwa wazee, kwenye hospitali na vituo vya afya.

Naye Mwenyekiti aliyechaguliwa, ndugu Elias Ngungat, amewashukuru wazee wenzake kwa kumwamini na kumpa dhamana ya kuwaongoza huku akiahidi kutumia uwezo alionao kuhakikisha anatetea haki za wazee wote bila kujali itikadi.

Aidha mwenyekiti huyo, ameishukuru serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kwa kuthamini kundi la wazee ambalo hapo awali kundi hilo lilikuwa halipewi kipaumbele.

Wajumbe wa Baraza la Wazee ngazi ya halmashauri, limaundwa na wajumbe watatu kutoka kila kata na kufanya Baraza la wazee halmashauri ya Arusha kuwa na jumla ya wajumbe 81 kutoka kata 27 za halmashauri hiyo.

PICHA ZA MATUKIO YA MKUTANO WA KUCHAGUA VIONGOZI.









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.