• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HOUSE OF HAPPINESS YAREJESHA FURAHA YA WATOTO WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU

Posted on: September 22nd, 2022

Na Elinipa Lupembe

Katika juhudi za kutokomeza ukatili dhidi ya watoto shirika lisilo la kiserikali la House of Happiness limezindua kituo cha kulelea watoto yatima na waishio kwenye mazingira magumu lengo likiwa ni kurejesha furaha iliyopotea kwa watoto hao kutokana na kupoteza wazazi pamoja hali ngumu ya maisha.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo hicho kilichopo Kijiji cha Loovilukunyi, Kata ya Kisongo, Mkurugenzi wa shirika la House of Happiness, Mohamed Kassim amesema kuwa lengo la kufungua kituo hicho ni kuwapatia watoto upendo kwa kuwapa malezi bora yatakayowarejeshea furaha na matumaini ambayo waliyapoteza kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wao.

Tunafahamu nchi yetu inakabiliwa na changamoto ya Watoto kuishi kwenye mazingira magumu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupoteza wazazi kunakosababisha Watoto kukosa haki zao za msingi, hivyo uwepo wa kituo hicho kutawawezesha watoto kupata huduma zote za msingi ikiwemo mavazi, malazi na chakula sambamba na kuwapatia elimu rasmi.

“Kila mtu anahitaji upendo, niwaombe wanajamii kushiriki kuwahudumia Watoto wenye mahitaji ili nao waishi kama Watoto wengine, kwa kuwa Watoto nao wanahitaji upendo ili kuwa na kizazi bora, ni furaha yangu kuwaona Watoto wakiwa na furaha pamoja na upendo”. Amesisitiza Kassim

Naye Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amewashukuru wadau wote walioshiriki katika kuwezesha kituo hicho kufanya kazi, kwa kuwa kituo hicho ni muhimu kwa Watoto wa kitanzania ambao walipoteza matumaini kutokana na sababu mbambali za maisha.

“Watoto hawa walikosa fursa katika Maisha yao lakini House of Happiness limeona umuhimu wa kuwapa huduma za msingi zitakazo warejeshea furaha na matumaini waliyoyapoteza, kurudisha ya mtu iliyopotea ni kitu kikubwa sana hata mbele za Mungu”. Amesema Mkurugenzi Msumi.

Aidha wananchi wa eneo hilo wamelishukuru shikika hilo kwa kujenga kituo cha Watoto wenye uhitaji na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano ili kufikia lengo la shirika na Serikali kwa ujumla wake la kuwahudumia watoto katika jamii.

“Watoto wanahitaji upendo wakati wote, hivyo wanapokosa mahitaji yao ya msingi kama vile chakula, maladhi na mavazi ni chanzo cha cha ukatili dhdi yao. Japo kuna hali ngumu ya maisha lakini kila mzazi anapaswa kufanya wajibu wake ili kuwawezesha Watoto kutimiza ndoto zao”. Alisema Simon Mollel, Mkazi wa Kijiji cha Loovilukunyi, Kata ya Kisongo

Naye Diwani wa kata ya Kisongo Mhe. Godson Loning’o amesema kuwa uwepo wa kituo hicho ni zawadi kubwa kutoka kwa mungu kupitia kwa shirika hilo la Hose of happiness na kuitaka jamii kuangalia mazingira ya watoto wao ili kuwapatia stahiki zao kama haki ya msingi.

Hata hivyo kituo hicho ambacho ujenzi wake ulianza mwaka 2019, kimezinduliwa kikiwa na Watoto kumi na moja (11) wakike watatu (3) na wakiume nane (8) na kinategemea kuhudumia watoto sitini na nne (64) wenye umri wa kati ya miaka mitatu (3) hadi kumi na mbili(12) kutoka sehemu yoyote ndani ya Tanzania bila kujali hali zao za kiafya.

ARUSHA DC,

TUPO KAZINI.

PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA UZINDUZI WA KITUO CHA WATOTO YATIMA NA WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU (HOUSE OF HAPPINESS)




Baadhi ya watoto wanaolelewa katika kituo cha House of Happiness wakiwa katika ukumbi wa kituo hicho wakati wa hafla ya uzinduzi


Mkurugenzi wa Kituo cha House of Happiness, Mohamed Kassim akifanya utambulisho wa wageni waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa kituo cha watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha Seleman Msumi (kushoto) akiteta jambo na mdhamini mwenza wa kituo cha House of Happiness mara baada ya uzinduzi wa kituo hicho







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.