• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Jamii imetakiwa kuachana na mila potofu dhidi ya watoto wa kike.

Posted on: February 25th, 2019

Na.Elinipa Lupembe.

Jamii halmashaiuri ya Arusha, imetakiwa kuachana na mila na desturi potofu dhidi ya watoto wa kike, badala yake kuungana kwa pamoja, kuhakikisha ulinzi na usalama wa mtoto, utakaowezesha mapambambano dhidi ya mimba za utotoni, mimba ambazo kimsingi  zinazima ndoto za watoto wa kike kwa asilimia kubwa.

Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Viti Maalum Taifa, Mheshimiwa Amina Mollel, wakati akizungumza wakati wa Mkutano wa robo ya nne wa Baraza la  Madiwani wa kuwasilidha taarifa za kata za halmashauri ya Arusha,  uliofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Amina, ametoa wito huo mara baada ya kuwasilishwa changamoto za ukatili kwa watoto wa kike hususani mimba za utotoni kwa baadhi ya kata, huku ikionekana mila na desturi bado ni tishio la utatuzi na udhibiti wa tatizo hilo.

Amefafanua kuwa, viongozi na jamii wanapaswa kufahamu kuwa, jukumu la kupambana na ndoa na mimba za utotoni,  si la serikali peke yake, kazi ya serikali ni kuandaa sera rafiki, lakini jamii ndio watekelezaji wa sera hizo, hivyo ni jukumu la viongozi hao, kuungana kuelimisha jamii, kufahamu athari kubwa za mimba za utotoni kiafya, kisaikolojia, kiuchumi na kimtazamo pia.

Amewata madiwani hayo, jambo hilo kuwa agenda ya kudumu kwenye vikao vyao, kuanzia ngazi ya familia, kitongoji, vijiji, kata na hata wanapopata nafasi ya kuhudhuria kwenye vikao vya mila, kwa kuwashirikisha viongozi wa mila kupambana na ukatili dhidi ya watoto wa kike ikiwemo ndoa na mimba na ndoa za utotoni.

" Kila mnapokaa kwenye vikao vyenu, zungumzieni tatizo na athari za ndoa na mimba za utotoni, washirikisheni viongozi wa mila, umuhimu wa mtoto wa kike kupata elimu, hata mimi nisingepata fursa ya kusoma, nisingekuwa mbunge, palilieni ndoto za watoto wa kike na sio kuzikatisha" amesema mbunge Amina kwa hisia kubwa.

Naya Afisa Elimu Msingi, halmashauri ya Arusha, Hossein Mghewa, amesema kuwa, licha serikali kuweka sheria kali lakini changamoto kubwa bado lipo ndani ya jamii yenyewe, changamoto inayotokana na mila na desturi inayolazimisha usiri wa kutokutoa ushirikiano kwenye mapambano dhidi ya ukatili wa mtoto wa kike.

Hata kama serikali inapambana kuwapata wahalifu hao, jamii imekua ikiwaficha watuhumia wa kesi hizo,  kwa kukubaliana kumaliza kesi nyumbani, huku wengine  wakiacha kufika mahakamini kutoa ushahidi hata kama aliyefanyiwa ukatili huo ni mtoto wake wa kumzaa, jambo ambalo linaharibu mwenendo wa kesi hizo kufika mwisho ili mahakama iweze kutoa haki ya mtoto.

" Hata zikifanyika juhudi za kuwakamata watuhumiwa na kuwafikisha mahakamani, kesi hushindwa kufika mwisho, familia nzima haifiki mahakamani kutoa ushahidi,hukutana na kumalizana wenyewe kimila,  na wakati mwingine wazazi wenyewe,  huwatorosha watoto" amesema Hossein

Hata hivyo bado serikali inaendelea kupanua wigo wa kuelimisha jamii hizo, kwa kuweka mikakati ya kupata wasaa wa  kuzungumza na watoto na wazazi kupitia Idara ya Uthibiti Ubora wa shule,  wakati wa ukaguzi wa shule ili kupata taarifa za siri kutoka kwao.

Mthibiti Ubora wa shule Fatuma Lema amethibitisha kuwa, kimeongezwa kipengele cha ukaguzi wa hali ya watoto shuleni hususani, mimba na ndoa za utotoni kwenye ukaguzi, kipengele kinachowalazimu kuzungumza na walimu , wanafunzi na wazazi, kwa lengo la kuelimisha na kutokomeza tatizo hilo.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.