• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

JAMII IMETAKIWA KUHAMASISHA WAJAWAZITO KUZINGATIA KUMEZA VIDONGE VYA FOLIC ACID NA MADINI CHUMA CHINI YA WIKI 12 ZA UJAUZITO.

Posted on: May 30th, 2023

Na Elinipa Lupembe 

Jamii imetakiwa kuwahasisha kina mama wajawazito halmashauri ya Arusha kuzingatia umezaji wa vidonge vya Madini Chuma na Folic acid,wanavyopewa kipindi cha chini ya wiki 12 za ujauzito pindi wanapohudhuria kliniki kwa wakati.

Rai hiyo imetolewa na Afisa Tarafa ya Mukulat Hudhaifa Rashid kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Arumeru ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe wilaya, kwenye kikao cha tathmini ya Lishe kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2022/2023 kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Arusha.

Mwenyekiti huyo ametoa rai hiyo, kufuatia taarifa ya Afya ya Uzazi na Mtoto,  iliyobainisha kuwepo kwa vifo vya watoto wakati wa kujifungua vinavyosababishwa na ulemavu wa mgongo wazi na tumbo nje, unaosababishwa ukosefu virutubisho, unaotokana na wajawazito kutokuzingatia kumeza vidonge vya Folic acid na madini chuma.

Ameitaka jamii kuwahamasisha wajawazito kuzingatia kuhudhuria kliniki kwa wakati na kuwakumbusha umezaji wa vidonge vyote wanavyopewa kwa kuwa ni muhimu katika hatua zote za ukuaji wa mwili wa mtoto akiwa tumboni na kushindwa kumeza vidonge hivyo kunaongeza hatari ya kumpoteza mtoto wakati wa kujifungua.

"Licha ya kwamba serikali inapambana kukabiliana na vifo vya watoto wakati wa kujifungua, bado kuna vifo vinavyotokana na uzembe wa wajawazito wenyewe, jambo ambalo si zuri sana kwa jamii na Taifa kwa ujumla, kunao uwezekano wa kuzuia vifo hivyo kama jamii na wajawazito wataamua" Amefafanua  Rashid 

Akizungumza wakati wa kuwasilisha taarifa hiyo, Mratibu wa Afya ya Uzazi  na Mtoto, Sista Bujiku Butolwa, amesema kuwa 38% ya wajawazito huchelewa kuanza kliniki na kukosa kupata vidonge vya Folic Acid na madini chuma, vidonge ambavyo, mama mjamzito anatakiwa kumeza chini ya wiki 12 za ujauzito jambo linalosababisha watoto kuzaliwa wakiwa na ulemavu wa hali ya juu, unayosababisha vifo.

Hata hivyo Bujiku ameweka wazi, umuhimu wa vidonge vya Folic acid kwa wajawazito chini ya wiki 12 kuwa, ina Vitamin B9 inajumuisha dutu mbili zinazosaidia afya ya mwili, utengenezwaji wa seli hai nyekundu za damu, utengenezaji na ukarabati DNA na RNA ambazo ni dutu muhimu za jeni, husaidia mgawanyiko wa haraka wa seli hai katika mchakato wa ukuaji pamoja na kuimarisha afya ya ubongo, hususani kwa ukuaji wa mtoto aliye tumboni.

Naye Afisa Lishe halmashauri ya Arusha, Dotto Milembe ameweka wazi kuwa, vidonge vya Folic Acid sio dawa bali ni tiba lishe ambayo imetengenezwa maalumu kwa ajili ya wajawazito kutokana na hali ya wajawazito wengi kushindwa kula baadhi ya vyakula hivyo vidonge vya Folic acid na madini chuma, vimetengenezwa kama mbadala wa virutubisho vinavyotokana na aina nyingi ya vyakula.

"Vidonge vya Folic Acid na madini chuma,  ni mbadala ya virutubisho vya aina nyingi vyenye umuhimu mkubwa katika hatua zote za kujenga mwili na akili ya mtoto kwa kuzingatia hatua zote ukuaji wa mtoto akiwa tumboni" Amefafanua Doto

Kikao cha tathmini ya Lishe, kwa kipindi cha robo ya tatu mwaka wa fedha 2022/2023 na hufanyika kila robo ya mwaka wa fedha, lengo likiwa ni kufanya ufuatilia wa watoto wenye utapiamlo kuanzia mama mjamzito, mtoto akiwa tumboni, kipindi cha kuzaliwa, watoto wa miaka 0 - 5, kinamama wanaonyonyesha, wanafunzi pamoja na jamii kwa ujumla wake.

"ARUSHA DC Ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
#KaziIendelee


















 


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.