• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

JAMII IMETAKIWA KUFAHAMU UMUHIMU WA KINGA TIBA YA KICHOCHO NA MINYOO KWA WATOTO

Posted on: March 3rd, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Jamii imetakiwa kutambua umuhimu ya kinga tiba ya magonjwa ya kichocho na minyoo inayotolewa na serikali kwa watoto wa kuanzia umri wa miaka 5 mpaka 14, ikiwa na kusudi la kuwakinga na kuwatibu watoto dhidi ya magonjwa  ya kichocho na minyoo tumbo, magonjwa ambayo yana athari kubwa kwa afya za watoto pamoja na kuathiri makuzi yao.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa halmashauri ya Arsuha, Mheshimia Ojung'u Salekwa wakati akizindua zoezi la siku mbili la utoaji wa vidonge vya kinga tiba dhidi ya magonjwa ya kichocho na minyoo tumbo kwa watoto wa  kuanzia umri wa miaka 5 mpaka 14 katika halmashauri hiyo, uzinduzi uliofanyika shule ya msingi Naurei kata ya kiutu.

Mwenyekiti Salekwa amesema kuwa ,serikali inatambua kuwa kati ya magonjwa yanaochangia udumavu wa afya kwa watoto ni pamoja na minyoo tumbo na ugonjwa wa kichoo, magonjwa yanayotokana na mazingira wanayotumia watoto kucheza, hivyo ni vema kuzingatia kuwapatia dawa za kinga ambazo zipo na hutolewa na serikali bure.

"Wazazi na walezi mnatakiwa kuunga mkono jitihada za serikali za kuhakikisha watoto wetu wanapata kinga tiba dhidi ya kichocho na minyoo, kwa kuwa magonjwa hayo yanadumaza afya na ukuaji wa mtoto, na baadaye kumuathiri mtoto kiakiali na kisaikolojia pia"amesema Mwenyekiti huyo.

Hata hivyo Mganga Mkuu halmashauri ya Arusha, Dkt. Petro Mboya, amesema kuwa halmashauri ya Arusha, inategemea kutoa kinga tiba ya magonjwa ya minyoo na kichocho kwa  jumla ya watoto 89,914 wa  kuanzia miaka 5 mpaka 14, walioandikishwa shule na wale wasioandikishwa shule, zoezi hilo likifanyika kwenye shule zote za msingi 163 za halmashauri ya Arusha, ikiwemo shule 96 za serikali na shule 67 za binafsi.

Dkt. Mboya ambainisha kuwa magonjwa ya minyoo na kichocho yana madhara makubwa katika makuzi ya mtoto, kwa kuwa minyoo hufyonza chakula anachokula mtoto, na matokea yake mtoto huanza kudhoofika kiafya kutokana na lishe yote anayokula kushambuliwa na minyoo, hivyo ni vema kumkinga mtoto dhidi ya minyoo ili kuimarusha afya yake.

Hata hivyo Dkt. Mboya, aliwataka wazazi na walezi kuyapuuza maneno ya kubeza dawa hizo kuwa zina madhara kwa watoto, jambo ambalo kitaalamu si la kweli, dawa hizo ni salama na zinatibu na kukinga magonjwa hayo ya kichocho na minyoo ya tumbo, huku akifafanua kuwa ni kweli kuna baadhi ya watoto huweza kutapika au kujisiskia vibaya, jambo ambalo ni la kawaida kulingana na mwili wa mtoto, na kuyaita matokeo hayo ni maudhi madogo madogo yanayotokana na dawa na kutokuwa na madhara yoyote makubwa zaidi.

Nayr mwalimu mkuu, shule ya msingi Naurei, mwalimu Getrude Tarimo, amesema kuwa wamejiandaa vema kukamilisha zoezi hilo kwa kuhakikisha watoto wote, waliogpfika shuleni wanapatiwa kinga tiba hiyo, kwa kuzingatia maelekezo ya watalamu wa afya.

"Kabla ya kupatiwa dawa hizo, tumelekeezwa mtoto lazima awe amekula chakula na kushiba, tayari tumewapa watoto wetu chakula, huku zoezi la kugawa dawa likiendelea"amesema mwalimu Getrude

Zoezi hilo la kutoamKinga tiba ya kichoho na minyoo ni zoezi la kitaifa na hufanyika kila mwaka mara moja, lifanyika kwa muda wa siku mbili katika halamshauri ya Arusha huku jumla ya watoto 89,914 wakitegemea kupata kinga tiba hiyo.


Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Ojung'u Salekwa, akimnywesha vidonge mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi Naurei, ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa zoezi la siku mbili la kugawa dawa za Kinga Tiba ya magonjwa ya Kichocho na minyoo tumbo kwa watoto wa miaka 5-14 katika halamshauri ya Arusha.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.