Na. Elinipa Lupembe.
Jumla ya wanafunzi 858 wanaanza mitihani ya Taifa ya kuhitimu kidato cha sita mwaka 2022, huku wanafunzi 18, wakifanya mitihani ya kuhitimu vyuo vya Ualimu, kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Mtihani la Taifa (NECTA).
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mkurugenzi Mtendaji, na mwenyekiti wa Kamati ya Mitihani, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amesema kuwa, wanafunzi hao 858, wanafanya mitihani hiyo kwenye jumla ya shule za sekondari 11 na vyuo viwili vya Ualimu.
Aidha mkurugenzi Msumi, amewataka wasimamizi wote wa mitihani hiyo, kusimamia mitihani kwa uadilifu kulingana na kanuni, sheria na taratibu za mitihani ya Taifa, huku wakijiepusha na vitendo vya udanganyifu.
"Niwatake wasimamizi wote wa mitihani, kufanya kazi hiyo kwa uaminifu na uadilifu, huku mkiweka mbele maslahi ya Umma na wanafunzi hao, tambueni kuwa mmebeba dhamana ya vijana, ambao Taifa linawategemea na limewekeza rasilimali nyingi" amesistiza Mkurugenzi Msumi.
Naye Afisa Elimu Sekondari, Mwalimu Menard Lupenza amefafanua kuwa, katika halmashauri ya Arusha, jumla ya wanafunzi 877, wameanza mitihani wa Taifa wa kuhitimu kidato cha sita na vyuo vya ualimu mwaka 2022, kufuatia ratiba iliyotolewa na Baraza la Mtihani la Taifa - NECTA.
Aidha ametaja makundi ya wanafunzi wanaofanya mtihani mwka 2022, wanafunzi 859, wanafanya mtihani wa Taifa wa kidato cha sita, huku 18 wakifanya mitihani ya Ualimu.
"Wanafunzi 728 ni wa shule 'school candidate' wavulani ni 344 na wasichana 379, huku wanafunzi 136 ni wa kujitegemea 'private candidates' wavulana 76 na wasichana 69, na wanafunzi 18 watafanya mitihani ya Ualimu ambapo wavulana 12 na wasichana 6" amefafanua Afisa Elimu huyo.
Naye Mkuu wa shule ya sekondari Mringa, Mwalimu Salum Magaka, ameweka wazi kuwa watahiniwa, wameandaliwa vema kwa ajili ya kufanya mitihani hiyo ya Taifa na wanategemea watafanya vizuri katika matokeo yao.
Awali uongozi wa halmashauri ya Arusha, unawatakia kila la kheri wanafunzi wote wanaofanya mtihani wa Taifa wa kuhitimu kidato cha sita mwaka 2020, mitihani inayoanza tarehe 09.05.2022.
ARUSHA DC
KaziIendelee✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.