• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kaimu Mkuu wa wilaya ya Arumeru awataka wajumbe wa Bodi ya NGAUWSA kuweka mikakati ya kutafuta lita milioni 4.2 za maji

Posted on: March 27th, 2018

Wajumbe wa bodi mpya ya Mamlaka ya Maji Ngaramtoni (NGAUWSA) wametakiwa kuweka mikakati thabiti ya kupatikana kwa lita milioni 4.2 za maji, zinazotakiwa kutumika kwa siku moja na wakazi wa Mamlaka ya Mji mdogo Ngaramtoni.

Wajumbe hao wametakiwa kutafuta lita hizo za maji kufuatia Mamlaka ya Maji NGAUWSA kuzaliza maji kiasi cha lita milioni 2.8 kwa siku, huku mahitaji ya maji kwa siku moja kwa wakazi wa eneo hilo ni lita milioni 7.

Kufuatia uzalishaji huo wa chini ya kiwango cha uhitaji wa maji kwa jamii, kumesababisha changamoto kubwa ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi hao.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mpya Bodi ya NGAUWSA, mgeni rasmi Kaimu mkuu wa wilaya ya Arumeru, mhe. Idd Kimanta amesema kuwa, kazi kubwa ya Bodi ya NGAUWSA ni kuweka mikakati thabiti ya kutafuta namna ya kupata lita milioni 4.2 iki kufikia lita milioni 7 zinazohitajika na wakazi wa Ngaramtoni kwa siku.

Wajumbe hao wametakiwa kutafuta lita hizo za maji, kufuatia Mamlaka ya Maji Ngaramtoni kuzalisha maji lita milioni 2.8 kwa siku, huku mahitaji ya maji kwa siku moja ni lita milioni 7.

Kufuatia uzalishaji huo wa chini ya kiwango chabuhitaji wa maji kwa jamii, kumesababisha changamoto kubwa ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi hao.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mpya Bodi ya NGAUWSA, mgeni rasmi Kaimu mkuu wa wilaya ya Arumeru, mhe. Idd Kimanta amesema kuwa, kazi kubwa ya Bodi ya NGAUWSA ni kuweka mikakati thabiti ya kutafuta namna ya kupata lita milioni 4.2 iki kufikia lita milioni 7 zinazohitajika na wakazi wa Ngaramtoni kwa siku.

Ameongeza kuwa baada ya NGAUWSA kuanzishwa mwaka 2015 imefanikiwa kutoa huduma ya maji kwa asilimia 40% tu, huduma ambayo haiwafikia hata nusu ya wakazi, huku wakipambana kufikia mpango wa serikali wa kufikia asilimia 95% ya upatikanaji wa maji mijini ifikapo 2010.

"Ndugu zangu wajumbe wa bodi hii ya NGAUWSA mnakazi kubwa ya kufanya,ya kuhakikisha asilimia 50% zinapatikana ili kufikia lengo la serikali la asilimia 95% ifikapo mwaka 2020 pamoja na kutafuta lita milioni 4.2. ili kufikia lita milioni 7 zinazohitajika kwa siku na wananchi wenu" amesema Kimanta.

Aidha amewaasa wajumbe hao wa bodi kutambua kuwa, ili huduma ya maji iweze kupatikana na kufikia malengo, bodi ina jukumu la kutoa huduma za maji na kuifanya NGAUWSA kujiendesha kibiashara, kwa kuhakikisha watu wanalipia maji na kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.

Mheshimiwa Kimanta hakusita kuwashauri kuwa ili kufikia malengo ni vema kutumia changamoto ya huduma za maji kwa wananchi wa mamlaka ya mji mdogo Ngaramtoni na zile zinazoikabili mamlaka ya maji NGAUWSA zigeuzwe kuwa fursa.

Awali Kaimu mkuu wa wilaya Kimanta, amemkabidhi kila mjumbe begi lenye vitabu venye miongozo na majukumu ya bodi, na kusema kuwa amewakabidhi silaha za kuhakikisha usalama wa afya za wananchi wao, kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama, ambayo ni kinga ya magonjwa ya mlipuko.

Naye Mwenyekiti wa Mamlaka ya mji mdogo Ngaramtoni mhe. Elias Munisi amesema wajumbe wote wa mamlaka wako tayari kutoa ushirikiano kwa Bodi hiyo ili kuhakikisha maji safi na salama yanapatikana kwa wananchi wote wa Mamlaka bila kujali tofauti za kitikadi.

Hata hivyo meneja wa NGAUWSA, Clayson Kimaro amesema kuwa, wanamatarajio makubwa ya kupatikana kwa lita zaidi ya milioni 3 kwa siku ifikapo mwishoni mwa mwaka huu 2018, baada ya mradi wa maji Ngaramtoni ulio katika hatua za mwisho na mradi wa maji wa vijiji vitano ulio katika hatua za awali, unaotegemea kukamilika mwezi Novemba, 2018.

Kimaro ameendelea kufafanua kuwa, kukamilika kwa miradi hiyo, kutaongeza usambazaji wa maji kwa wateja katika eneo la Mamlaka ya Mji mdogo Ngaramtoni.

Mwenyekiti wa Bodi ya NGAUWSA, John Sirikwa amesema kuwa, licha ya Changamoto zinazoikabili mamlaka hiyo, wao kama wajumbe wa Bodi wamejipanga kushirikiana na viongozi, watalamu na wananchi ili kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa asilimia 95% ifikapo mwaka 2020 kama agizo la serikali ya awamu ya tano linavyotaka.

Sirikwa Amesema kuwa wamechukua ushauri wa mkuu wa wilaya wa kugeuza changamoto zote kuwa fursa, na kuifanya NGAUWSA kuwa mamlaka ya kutoa huduma kwa wananchi yenye mikakati thabiti ya kibiashara.

Bodi ya mamlaka ya maji NGAUWSA imezinduliwa leo ikiwa na jumla ya wajumbe saba, baada ya mamlaka hiyo kusajiliwa na wajumbe wake kupatiwa mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo juu ya majukumu yao katika uendeshaji na Mamlaka hiyo ya maji.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.