• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAIRUKI AAGIZA USIMAMIZI WA HUDUMA ZA AFYA KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA..

Posted on: June 13th, 2023

Na James Mwanamyoto, ARUSHA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Angellah Kairuki amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Wilaya na Waganga Wafawidhi wa vituo vya afya nchini kuongeza uwajibikaji katika usimamizi wa huduma za afya.

Mhe. Kairuki ametoa maelekezo hayo leo jijini Arusha alipokuwa akifungua kikao kazi cha watendaji hao wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Waratibu wa UKIMWI na Wakurugenzi Wasaidizi wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI kinacholenga kuongeza ufanisi kiutendaji. 

Waziri Kairuki amewataka watendaji hao kuhakikisha fedha zilizotolewa na Serikali katika sekta ya afya zinatumika ipasavyo katika kuboresha huduma za afya nchini.

“Ni vema mkahakikisha kwamba vituo vyote vya kutolea huduma za afya vilivyokamilika vinaanza kutoa huduma ili kuwapunguzia gharama na adha wananchi ya kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya kufuata huduma,” Mhe. Kairuki amesisitiza.

Aidha, Mhe. Kairuki amesema moja ya kigezo kitakachotumika kupima utendaji kazi wa watendaji hao ni pamoja na kusimamia kikamilifu  vituo vya afya kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mhe. Kairuki amewataka watendaji hao kuhakikisha mifumo iliyopo ya kiutendaji inafanyakazi kwa ufanisi katika sekta ya afya ukiwepo Mfumo wa Dharula wa Rufaa wa M-Mama uliozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Mwezi Aprili 2022 ambao umepunguza vifo vya mama na mtoto, akitoa mfano kwa mkoa wa Shinganga ambao vifo kwa upande wa akina mama vimepungua kwa asilimia 38 na kwa watoto ni asilimia 45.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Denis Londo amewataka washiriki wa kikao kazi hicho kuweka mkakati madhubuti wa kulinda na kuendelea kuboresha afya ya kila mtanzania.

Pia, Mhe. Londo amesisitiza uwajibikaji wa watendaji hao wa afya katika kusimamia miradi ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa mstari wa mbele kutafuta fedha ili wananchi wanufaike na huduma za afya.

Awali, Naibu Katibu Mkuu-TAMISEMI anayeshugulikia Afya Dkt. Charles Mahera amesema kikao kazi hicho cha siku mbili kina lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji na uelewa wa pamoja watendaji hao wa sekta afya katika utekelezaji wa utoaji wa huduma za afya katika ngazi ya msingi kwenye Halmashauri.

Kadhalika, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella amewapongeza watendaji hao wa sekta ya afya kwa kuendelea kuwahudumia wananchi katika maeneo yao ya kazi.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.