• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA YAAGIZA UJENZI WA BWENI LA WAVULANA NA UZIO SEKONDARI OLDONYOWAS

Posted on: November 13th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za mitaa, wamemuagiza Waziri, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kujenga bweni la wavulana apmaoja na uzio kwenye shule ya sekondari Oldonyowas, halmashauri ya Arusha, wakati kamati hiyo ya Bunge, ilipotembelea shuleni hapo, kukagua miradi inayotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF.

Wajumbe wa Kamati hiyo, wamefikia uamuzi huo baada ya kupokea maombi kutoka kwa wanafunzi, wazazi na viongozi wa kijiji na kata ya Oldonyowas, kutoa ombi kwa kamati hiyo, kujengewa bweni la wavulana na uzio wa shule, kutokana na wanafunzi wengi wanaosoma shuleni hapo, wanatoka kwenye familia za wafugaji, familia ambazo wana tabia ya huhama makazi yao, wakati wa ukame ili kufuata malisho ya mifugo yao, na kusababisha watoto wengi kuacha shule kufuata familia zao.

Akizungumza baada ya kukagua na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Utawala na Serikali za mitaa, Mheshimiwa Abdalah Kalembo, ameweka wazi kuwa, kamati hiiyo imeona umuhimu wa kujenga bweni la wanafunzi wavulana shuleni hapo, ili kuwapa wigo mpana na watoto hao kutika familia za wafugaji, kuwa na mazingira rafiki ya kusomea, tofauti na mazingira ya nyumbani ambayo familia zao huishi kwa kuhama hama.

"Kama alivyosema mheshimiwa Diwana wa Oldonyowas, watoto hawa wanatoka kwenye familia za wafugaji, isingekuwa kuna bweni hapa, watoto hawa wasingekuwepo shuleni hapa leo, wangehama na familia zao, ili kuhakikisha watoto wote wa familia za wafugaji wanapata haki ya kusoma, mheshimiwa Waziri, fanyeni utaratibu wa kujenga bweni la wavulana na uzio katika shule hii kwa haraka" amesisitiza Mwenyekiti wa Kamati Mheshimiwa Bulembo.

Hata hivyo, Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amekubali ombi na agizo hilo, na kusema kuwa, utaratibu wa kuanza ujenzi wa bweni la wavulana na uzio katika shule hiyo, utaanza mapema, kwa kuwa serikali ya awamu ya sita, imejipanga kupambana na adui ujinga kwa kuhakikisha watoto wanaotekea kwenye kaya zenye uhitaji, zinazohudumiwa na mradi wa TASAF zinapata elimu katika mazingira rafiki.

"Kupitia miradi ya TASAF serikali imejipanga kupambana na adui wa haki, anayesababishwa zaidi na ujinga, maradhi na umasikini, maadui hao wote wanaondolewa kupitia miradi ya TASAF, ujenzi wa bweni na uzio, utafanyika kwa haraka ili kunusuru watoto hawa wasiathirike katika masomo yao, kwa kuwa kipaumbeke cha serikali ni kuinua kipato cha kaya ambazo hazina uwezo, ili kuinua uchumi na ustawi wa kaya hizo" amesisitiza Waziri Mchengerwa.

Awali Diwani wa kata ya Oldonyowas, Mheshimiwa Kijana Saruni, licha ya kuishukuru serikali kwa kuona umuhimuwa wa wananchi wa watoto wa kijiji hicho kwa kuwapa miradi mingi ya TASAF, aliwasilisha mbele ya kamati hiyo ya Bunge, ombi la kupatiwa mradi wa ujenzi wa bweni la wavulana pamoja na uzio katika shule ya sekondari Oldonyowasi, kwa kuelezea matokeo yalionekana kwa muda mfupi kutokana na uwepo wa bweni la wasichana na kuongeza kuwa uwepo wa bweni la wavula utasaidia watoto wa jamii za kifugaji kusoma.

"Uwepo wa bweni la wasichana, umesaidia wanafunzi kuendelea na masomo, kungekuwa hakuna bweni, wanafunzi hawa wasingikuwepo shule leo wakati wa msimu wa ukame, watoto wengi wangekuwa wameondoka na wazazi wao, kwenda kutafuta malisho ya mifugo, tunaomba mtusaidie ujenzi wa bweni na kwa watoto wa kiume ili waweze kusoma kwa utulivu" amesisitiza Mheshimiwa Diwani.

Awali Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za mitaa, imetembelea kijiji cha Oldonyowas,  na kukagua miradi inayotekelezwa na TASAF awamu ya III, ikiwemo ujenzi wa jengo la utawala, vyumba vya madarasa, vyoo, nyumba mbili za walimu, mabweni mawaili ya wasichana,shule ya sekondari Oldonyowas, pamoja na mradi wa uhawilishaji fedha kwa kaya masikini na vikundi vya kuweka na kukopa.

Tangu mwaka 2014, TASAF awamu ya III na mpango wa kunusuru kaya masikini, imetekeleza katika vijiji 45 vya halmashauri ya Arusha na kuzifikia ya  jumla ya kaya 9,107, huku kaya hizo zikipokea fedha kwa mizunguko 28 na jumla ya shilingi bilioni 9.5 zilihawilishwa kwa walengwa jumla ya miradi 46 yenye thamani ya shilingi bilioni 2.1 ilitekelezwa katika sekta ya elimu, afya,  miundombinu ya barabara, uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia vikundi vya kilimo, ufugaji na utunzaji wa mazingira.

ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍


PICHA ZA MATUKIO YA ZIARA

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Utawala na Serikali za mitaa, wakikagua miradi ya miundombinu ya shule ya sekondari Oldonyowas, wakiongozwa na mwenyekiti wa  kamati Mhe. Abdala Kalembo na Waziri OR Menejimenti ya Utmishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamedi Mchengerwa, wakati wa ziara ya kamati hiyo, kukagua miradi inayotekelezwa na serikali kupitia TASAF awamu ya III.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Utawala na Serikali za mitaa, wakizungumza na wanafunzi wasichana wa shule ya sekondari Oldonyowas, wakati wa ziara ya kamati hiyo kijijini hapo kukagua miradi ya miundombinu ya shule ya sekondari Oldonyowas, wakiongozwa na mwenyekiti wa  kamati Mhe. Abdala Kalembo na Waziri OR Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Mohamed Mchengerwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Utawala na Serikali za mitaa, Mheshimiwa Abdalah Kalembo, akizungumza na hadhara ya wananchi wa kijiji cha Oldonyowas, halmashauri ya Arusha, wakati wa ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Mfuko wa maendeleo ya Jamii - TASAF awamu ya III, katika shule ya sekondari Oldonyowas.


Waziri Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa, akizungumza na hadhara ya wananchi wa kijiji cha Oldonyowas, halmashauri ya Arusha, wakati wa ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Mfuko wa maendeleo ya Jamii - TASAF awamu ya III, katika shule ya sekondari Oldonyowas.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Utawala na Serikali za mitaa, wakikagua mradi wa mabweni ya wasichana shule ya sekondari Oldonyowas, wakati wa ziara ya kamati hiyo, kukagua miradi inayotekelezwa na serikali kupitia TASAF awamu ya III.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.