• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Siasa CCM Arumeru, yaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo Arusha DC

Posted on: March 31st, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa Chama cha Mapinduzi, wilaya ya Arumeru, wamefanya ziara na  kukagua jumla ya miradi nane ya maendeleo inayotekelezwa katika halmashauri ya Arusha kufuatia utekelezaji wa Ilani ya Chama ya mwaka 2015 katika halmashauri hiyo.

Katika ziara hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Arumeru, ndugu Simon Ole Saning'o, wamekagua miradi yenye thamani ya takribani shilingi bilioni 12.5, katika sekta za Elimu, Afya, Maji na miundombinu ya barabara.

Wajumbe hao wa Kamati ya Siasa, wameonesha kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri hiyo, baada ya kubaini ubora wa miradi hiyo kwa kulinganisha na thamani ya fedha zilizotumika' value for mone',  huku wakiwapongeza wananchi wa halmashauri ya Arusha kwa kujitoa kwa hali na mali kuchangia utekezaji wa maendeleo katika vijiji na kata zao.

Aidha Mwenyekiti Saning'o amesema kuwa, kati ya miradi nane iliyotembelewa miradi miwili ya ujenzi ya vyumba vinne vya madarasa na ofisi ya walimu shule ya sekondari Kiranyi na vyumba vitatu  vya madarasa shule ya sekondari Lengijave, unatekelezwa kwa juhudi za wananchi mpaka kukamilika huku miradi mingine miwili wananchi wameichangia pia licha ya kupata fedha kutoka serikalini na wafadhili.

"Niwapongeze wananchi wa halmashauri ya Arusha, kwa kutambua umuhimu wa kutekeleza maendeleo kwenye maeneo yenu kwa faida yenu na vizazi vyenu, juhudi hizo zinaonyesha uwezo wa taifa letu kuanza kujitengemea na kuacha kutegemea misaada kutoka nje" amesema Saning'o

Hata hivyo Mwenyekiti Saning'o amesema kuwa licha ya asilimia kubwa ya miradi kutekelezeka kwa wakati,  Kamati hiyo imebaini changamoto ya ucheleweshwaji wa ukamilishaji wa miradi ya maji ya vijiji kumi, iliyokuwa ikifadhiliwa na Benki ya Dunia, miradi ambayo mpaka sasa haijakamilika na kuitaka serikali kukamilisha miradi  ili wananchi waweze kupata maji.

Naye Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Arusha, Angela Mvaa amethibitisha kuwa miradi hiyi ya maji ilianza mwaka 2013 na kusimama kwa muda mrefu, lakini  kwa sasa Serikali ya awamu ya tano imeanza kutoa pesa kwa ajili ya ukamilishaji wa miradi hiyo licha ya changamoto nyingi za mabadiliko ya kimazingira na tabia nchi kukabili utekelezaji wa miradi hiyo.

Hata hivyo Mvaa ameongeza kuwlicha ya changamoto za kuchelewa kwa miradi hiyo, mpaka sasa jumla ya miradi ya vijiji vitani kati ya kumi imekwishakamilika na tayari wananchibwameanza kupata maji, huku miradi ya vijiji vingine vitano ikiwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo amefafanua kuwa, miradi yote ilikaguliwa  na Kamati hiyo ya Siasa imetekelezwa na fedha kutoka Serikali Kuu, fedha za mapato ya ndani, kwa kushirikiana na wadau wa mbalimbali wa  maendeleo wa ndani na nje ya nchi, mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na nguvu za wananchi kwa usimamizi thabiti wa watalamu wa halmashauri hiyo kisekta.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo umekwenda sambamba na ahadi ya mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, alipoingia madarakani kufuatia Ilani ya chama kinachoongoza serikali Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015.

Mvaa ameitaja miradi iliyotembelewa na Kamati hiyo ya Siasa,  ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Manyire, mradi wa ujenzi wa maktaba na ukarabati wa bwalo la chakula shule ya sekondari Mlangarini, ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na ofisi shule mpya ya sekondari Manyire.

Ujenzi wa madaraja Laroi na Mirongoine, ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa shule ya sekondari Kiranyi, ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya sekondari Lengijave, mradi wa maji wa vijiji vitano maarufu kama WaterAid, mradi wa maji Loovilukuny na mradi wa kivuko Matevesi.

Halmashauri ya Arusha inawataka wananchi kuendelea kuiamini na kuiunga mkono Serikali yao kwa kuchangia maendeleo katika maeneo yao, huku wakijikita katika kufanya kazi kwa bidii kwa kuwa ndio msingi wa maendeleo, kuelekea uchumi wa kati ifikapo 2025.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.