• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA SIASA MKOA WA ARUSHA YARIDHISHWA NA UTEKELZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO ARUSHA DC

Posted on: March 19th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa mkoa wa Arusha wameridhishwa na utekelazaji wa miradi ya maendeleo, inayotekelezwa na fedha za Umma, katika halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.

Wajumbe hao wameridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo, waliyokiri inabainisha ubora wa mradi kwa kulinganisha na thamani ya fedha iliyotumika, wakati wa ziara ya kutembelea miradi 8 yenye thamani ya shilingi milioni 914.3,  katika sekta ya Elimu, Afya pamoja na miundombinu ya barabara, katika halmashauri ya Arusha mapema wiki hii..

Aidha Wajumbe hao wamefurahishwa zaidi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo, inayotokana na fedha za mapato ya ndani ya halmashauri ya Arusha, ikiwemo mradi wa shule ya mchepuo wa kiingereza Enaboishu Academy, miradi ambayo imekamilika kwa wakati na kwa kuzingatia bajeti iliyotengwa na Serikali kwa mwaka husika.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa mkoa wa Arusha, Moloimet Olemoko amebainisha kuwa, Kamati hiyo ya Siasa, imeridhishwa na hali ya miradi yote iliyotembelewa na kuongeza kuwa hii ni kuonesha kazi nzuri inayofanywa na serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na mheshimiwa Rais mama Samia Suluhu Hassan.

"Miradi ni mizuri, imetekelezwa kwa viwango na ubora unaokubalika, imetekelezwa kwa kuzingatia Ilani ya Chama cha Mapinduzi pamoja na maenelekezo yanauotolewa na serikali, ikiwa na lengo la kuwahudumia watanzania wote bila kujali itikadi zao, tunaponheza sana juhudi za Mheshimiwa Rais, Mama yetu Samia" amesema Olemoko.

Naye mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango amesema kuwa,  utekelezaji wa miradi hiyo, unapambanua juhudi za serikali  ya awamu ya sita kisekta, kwa kupanua wigo katika sekta ya elimu kwa kujenga vyumba vya madarasa  pamoja na kuongeza vituo vya afya katika wilaya ya Arumeru.

Aidha amewataka walimu kuongeza bidii katika kazi ya kufundisha sambamba na kuwa wabunifu katika kuwafundisha wanafunzi, kwa kuwa  taifa limejikita kipambana na adui ujinga, umaskini na maradhi hivyo, watoto wanapaswa kuwapata elimu bora itakayo likomboa taifa, zaidi amewaomba wananchi kutunza miundombinu iliyojengwa kwenye maeneo yao, ili iweze kutumiwa na vizazi vijavyo.

"Serikali  ya awamu ya sita imewekeza fedha nyingi kwenye sekta ya Elimu ambapo  Wilaya ya Arumeru imepata fedha za kujenga vyumba vya madarasa 170 pamoja na shilingi bilioni 2.4 za ujenzi wa miundombinu ya barabara, lengo likiwa ni kuboresha huduma za jamii katika wilaya yetu ya Arumeru" Amesisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Hata hivyo, Mkuu wa shule ya  Sekondari Kimnyaki, mwalimu, Paschal Ginana, ameishukuru serikali  kwa kuwekeza nguvu nyingi kwenye sekta ya elimu, nguvu ambayo imewesha wanafunzi kujifunza katika mazingira bora huku walimu wakirahisishiwa tendo la kufundisha kupitia ubora wa vyumba hivyo vya madarasa.

Jumla ya miradi 8 yenye thamani ya shilingi milioni 914.3, imetembelewa na kamati hiyo ya siasa ikiwemo miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, ujenzi wa shule ya mchepuo wa kiingereza Enaboishu Academy, ujenzi wa Vituo vipya vya Afya Mwandeti na Oloirieni, pamoja na muindombinu ya barabara.

ARUSHA DC

KaziInaendeleaa✍✍✍✍









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.