Angela Msimbira TABORA
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughukia Elimu Dkt.Charles Msonde amewataka viongozi wa Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanasimamia na kukamilisha ujenzi wa madarasa 8000 ifikapo Disemba 15,2022 ili wanafunzi wote wanaochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023 wanapata nafasi.
Ametoa kauli hiyo leo Novemba 18, 2022 wakati akikagua utekelezaji wa maelekezo ya Serikali hususani kwenye miundombinu ya shule za Sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge na Uyui Mkoani Tabora.
Dkt. Msonde amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha kiasi cha shilingi biilioni 160 kwa ajili ya kuhakikisha madarasa 8000 yanajengwa katika shule za Sekondari kwa lengo la kuhakikisha watoto wote wanaochaguliwa kujiunga na kidato cha Kwanza mwaka 2023 wanapata nafasi ya masomo.
Dkt. Msonde amesema watoto waliomaliza darasa la saba mwaka huu ni matokeo ya sera bila ada iliyoanzishwa mwaka 2016 na ndio wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023, hivyo lengo la Serikali ni kuhakikisha madarasa yanajengwa kwa ajili ya kutatua changamoto ya madarasa nchini.
Amesema kutokana na sera hiyo, kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi kujiunga na elimu ya msingi hali hii imepelekea changamoto ya miundombinu ya madarasa kwenye shule za Sekondari nchini hivyo Serikali kwa kuliona suala hilo imeweka mkakati wa kuhakikisha miundombinu ya madarasa inajengwa na kukamilika kwa wakati.
“Mwaka 2021 kulikuwa na Changamoto ya madarasa ambapo watoto waliokuwa wanatakiwa kujiunga na kidato cha kwanza walikuwa zaidi ya 970,000, ambapo uwiano wa wanafunzi wanaomaliza shule kuwa wachache ukilinganisha na wale wanaojiunga na kidato cha kwanza “amesema Dkt.Msonde
Ameendelea kufafanua kuwa mwaka 2023 wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza ni milioni 1.1 wakati wanaotoka ni 430,000, kunatofauti ya wanafunzi 600, hivyo serikali iliamua kutoa kiasi cha shilingi bilioni 160 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 8000 ili kuongeza madarasa kwenye shule za Sekondari
Amesema kwa upande wa tabora Serikali itajenga madarasa 565 lengo likiwa ni kukabiliana na wanafunzi watakaojiunga na Kidato cha kwanza Mwaka 2023
Kuhusu suala la kuondoa tatizo la watoto kutembea umbali mrefu kufuata masomo Dkt.Msonde amesema Serikali imeweka mkakati wa kulitatua hilo kupitia mradi wa kuboresha elimu ya sekondari (Sequip) ambapo unatarajia kujenga shule za sekondari mpya 1026 ndani ya miaka mitano ambapo shule 26 zitajengwa ambapo kila mkoa kutakuwa na shule moja na shule 1000 zitajengwa katika kila kata.
Aidha amesema katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule 184 ambapo kila Halmashauri inapewa shule moja hivyo serikali imedhamiria kumpunguzia mtoto kutembea umbali mrefu kufuata masomo.
CHANZO: TAMISEMI.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.