Na. Elinipa Lupembe.
Kikao maalum cha Tathmini ya Hali ya Lishe, ngazi ya kata, halmashauri ya Arusha, kwa kipindi cha robo ya pili, 2021/2022 ya kuanzia mwezi Oktoba mpaka Desemba 2021, kimefanyika kwenye ukumbi wa Mwenyekiti halmashauri ya hiyo.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa matokeo ya Tathmini ya Hali ya Lishe ngazi ya kata, Afisa Lishe halmashauri ya Arusha, Doto Milembe, ameweka wazi viashiria 6 vya vinavyozingatiwa kitaifa, katika kufanya tahmini ya Lishe katika ngazi ya kata.
Aidha amesema kuwa, kwa kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2021/2022, kwa kuzingatia vigezo 6 vya kitaifa, halmashauri ya Arusha, imepata asilimia 87 kwenye kigezo cha vijiji kuadhimisha Siku ya afya ya Lishe, asilimia 73.9 kigezo cha vijiji vilivyoabandika taarifa za Lishe kwenye mbao za matangazo, asilimia 0.9 ya watoto waliogundulika kuwa na utapiamlo mkali, asilimia 100 idadi ya watoto wenye utapiamlo mkali waliokwenda kupata matibabu kwenye vituo vya afya na asilimia 100 kigezo cha idadi ya kaya zenye wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano, zilizotembelewa na Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii, huku asilimia 45 tu ya vijiji vyenye sheria ndogo za masuala ya Lishe ili kupambana na Utapiamlo mkali.
"Changamoto zinaathiri hali ya Lishe katika halmashauri yetu, ni pamoja na baadhi ya vijiji kushindwa kubandika taarifa za Lishe kwenye mbao za matangazo na baadhi ya vijiji kutokuwa na sheria ndogo za masuala ya lishe na kuoambana na utapiamlo mkali, tukifanikiwa kupandisha vigezo hivi tutakuwa kwenye hali nzuri kitaifa" amefafanua Afisa Lishe huyo.
Naye Kaimu Mkurugenzi, halmashauri ya Arusha, Paulus Kessy, amesema kuwa sheria ndogo ziko kwenye mchakato na tayari wajumbe wa Baraza la Madiwani wamepitisha rasimu ya sheria ndogo, na kuwataka Maafisa Watendaji wa kata, kusimamia na kuhakikisha kila kijiji kinabandika taafifa za lishe kwenye mbao za matangazo na kuzipitia kila mwezi.
Hata hiyo Maafisa Watendaji wa kata wamekubaliana kuendelea kuwasimamia wahudumu wa afya ngazi ya jamii pamoja na kufuatilia tathmini ya Lishe katika kata zao kwa kuzingatia vigezo vya kitaifa, kwa kuendela kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa lishe bora pamoja na madhara ya lishe duni.Katika mkutano huo, Maafisa watendaji hao, wametakiwa pia kuendelea kuhamasisha wanawake kupima na wasichana kupata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi, chanjo inayotolewa bure katika vituo vyote vya afya pamoja na Kliniki inayotembea, 'mobile clinic'.
Kikao maalum cha Lishe, kinafanika kila robo ya mwaka wa fedha na kinajadili taarifa ya tahmini ya hali ya utekel3zaji wa shughuli za Lishe ngazi ya kata kwa kuzingatia vigezo 6 vilivyoainishwa kitaifa.ARUSHA DCKaziInaendelea✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.