• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KILA MWANAJAMII KUSHIRIKI KIKAMILIFU KUZUIA UKATILI WA KINGONO

Posted on: April 16th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Kila mwanajamii ametakiwa kushiriki kikamilifu kupambana na kuzuia ukatili wa kingono kwa watoto wa kiume na wa kike,unaoendelea ndani ya familia na jamii zetu, ukatili ambao unasababiha athari kubwa kwa jamii, ili kuijenga jamii bora yenye haki na usawa.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, wakati wa kikao cha mwaka cha wadau wa kupinga Ukatili wa kingono kilichoandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Center for Women, Children and Youth Development (CWCD) kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Mkurugenzi Msumi amesema kuwa, jamii inatakiwa kuwa karibu na watoto wao ili kuwapa elimu itakayobadilisha fikra na maisha yao hata watakapokuwa wakubwa.

“Wazazi wamekuwa ‘bize’ sana na shughuli zingine za Maisha na kusahau majukumu yao kama wazazi ya kuwalea watoto katika njia sahihi ya makuzi na malezi ya watoto, wanakosa muda wa kuzungumza nao kuhusu masuala ya ukatili hali inayopelekea matukio ya ukatili wa kingono kuongezeka”. Amesema Mkuregenzi Msumi.

Aidha amewataka wanafunzi walioshiriki katika kikao hicho na kupata mafunzo ya namna ya kuzuia ukatili wa kingono kwa kutoa taarifa sehemu husika hasa kwa viongozi wa ngazi mbalimbali kuwa mabalozi wa kusambaza elimu hiyo kwa wanafunzi wenzao huku akiwataka wazazi kutenga muda wa kuzungumza na watoto wao kuhusu masuala ya ukatili.

Hata hivyo, Mkurugenzi Msumi amewaagiza watendaji wa Kata zote za halmashauri yake kuteua wazazi au walezi wa kiume wanne kila Kata kuwa baba wa zamu (Father on Duty) ili kuboresha hatua za kuongea na watoto wa kiume na kuwapatia elimu hasa watoto walio katika kipindi cha balehe kupitia maabara za watoto wa kiume (boys VAC lab) zitakazoanzishwa kwenye shule za msingi.

Kwa upende wake Mkurugenzi wa shirika la CWCD Hindu Mbwego, ameitaka jamii kuwajengea watoto wa kiume uwezo wa kujieleza na kufichua vitendo vya ukatili wa kingono wanavyotendewa na kuepukana na dhana iliyopo ya mtoto wa kiume hatakiwi kuonyesha udhaifu.

“Tukiwajengea watoto wakiume uwezo wa kujielezea yale yanayowasibu tutaweza kuwanusuru na vitendo vya ukatili wa kingono na kuijenga jamii bora Zaidi”. Amesisitiza Mama Hindu.

Aidha, wadau mbalimbali wa kupinga Ukatili wa kingono walioshiriki katika kikao hicho wamelishukuru shirika hilo kwa kuanzisha mradi huo ambao unalenga kuwakomboa watoto wa kiume dhidi ya ukatili wa kingono ambapo kila mmoja kwa nafasi yake ameahidi kutoa ushirikiano katika hatua zote za upelelezi na ufuatiliaji wa matukio ya kingono pale yanapotokea.

Akizungumza katika kikao hicho, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Arumeru Mwamini Kazema, amesema kuwa kuna haja ya kuwajengea watoto uwezo na ujasiri wa kujieleza ili kuwawezesha kupata haki yao ya msingi pale wanapofanyiwa ukatili wa kingono kwani Mhanga wa tukio ndiye shahidi wa kwanza katika kesi hivyo inapotokea mtoto kupata hofu wakati wa kujieleza inapelekea kutoa ushahidi ambao haujajitosheleza.

“Tunaomba vyombo husika kufanyia kazi kwa haraka matukio ya Ukatili wa kingono ili kesi zinazotokana na matukio hayo zisichukue muda mrefu kutoa hukumu ili watoto wapate haki zao na kuepusha mianya ya rushwa au usuluhishi wa kifamilia kutokea” alisisitiza mwalimu wa shule ya Msingi Ilboru Rozina kawahe.

Awali, Shirika hilo la CWCD linatekeleza Mradi wa kuwawezesha watoto wa kiume kuzuia ukatili wa kingono chini ya ufadhili wa shirika la Foundation Civil Society (FCS) katika kata sita za Olturoto, Kiutu, Kiranyi, Oltrumet, Moivo pamoja na Ilboru.

"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

#kaziinaendelea✍✍✍✍






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.