• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kiseriani wapata fedha za kujenga shule ya sekondari

Posted on: July 17th, 2018

Na. Elinipa Lupembe.

Kufuatia mpango mkakati wa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli, unaolekeza elimu ya msingi kuwa ni haki ya lazima kwa kila mtoto, na kwa sasa itaanzia darasa la awali mpaka kidato cha nne, wananchi wa kijiji cha Kiseriani kata ya Mlangarini halmashauri ya Arusha, wameunga mkono mpango mkakati huo wa Serikali kwa vitendo.

Wananchi hao wameamua kujenga shule ya sekondari ambayo haijawahi kuwepo kijijini hapo, tangu enzi na enzi ili watoto wao wapate elimu hiyo ya msingi ndani ya kijiji chao na kuwaondolea watoto wao ada ya kutembea umbali mrefu kwenda kupata elimu ya sekondari.                          

Wananchi hao wa Kiseriani,  wamefikia uamuzi huo makini, mara baada ya kupokea fedha kiasi cha shilingi milioni 150, kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe kama fidia ya shamba ambalo kijiji hicho kilitoa kwa chuo hicho.      

Licha ya  wananchi hao kukabiliwa na changamoto nyingine, wameamua kutumia fedha hizo kuwekeza kwenye elimu, kwa kujenga shule mpya ya sekondari, kwa kuwa watoto katika eneo hilo hulazimika kutembea mpaka kijiji cha Mlangarini kupata elimu ya sekondari, eneo ambalo lina umbali mrefu kijiografia.                        

Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera amesema kuwa, kwa mujibu wa miongozo ya serikali ya awamu ya tano,  ujenzi wa shule hiyo hautatumia wakandarasi na badala yake utatumia 'Force Account', utaratibu unaoruhusu kutumia 'local fundis' mafundi wa kijijini kwa kusimamiwa na kamati zilizochaguliwa na wananchi wa eneo hilo chini ya uangalizi wa watalamu wa halmashauri.

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa,  tayari wananchi wa kijiji cha Kiseriani wamesha chagua Kamati ya ujenzi na Kamati ya manunuzi, zitakazohusika na usimamizi wa hatua zote za ujenzi wa miundombinu ya shule hiyo na kuongeza kuwa majengo hayo yanatakiwa kukamilika, mwishoni mwa mwaka huu 2018.

"Kazi ya kamati hizi ni kusimamia hatua zote za ujenzi huku zikisimamia manunuzi ya vifaa kuanzia mwanzo mpaka kukamilika kwa ujenzi na tunategemea ujenzi huo kukamilika mapema mwaka ili Januari wanafunzi waanze kusoma hapo" amesema Mkurugenzi huyo.  

Aidha mkurugenzi Mahera amewataka wananchi wa kijiji cha Kiseriani, kushiriki kwa hali na mali na kuhakikisha ujenzi umekamilika kulingana na thamani ya fedha zilizopo 'value for money'.                                                      

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Kiseriani mheshimiwa Zebedayo Thomas amesema kuwa,  licha kuipongeza serikali ya awamu ya tano na Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha kwa kuungana nao,  kuhakikisha watoto wao wanapata elimu ya sekondari ndani ya eneo lao, amewaomba watalamu  kushirikiana nao wakati wote wa utekelezaji wa mradi huo.  

Juliana Lekeye mkazi wa Kiseriani amesema kuwa, kwa sasa watoto wa Kiseriani  wamepata neema kubwa, kutokana na ukweli kwamba, wamekuwa wakitembea umbali mrefu kwenda  shule ya Sekondari Mlangarini zaidi ya Kilomita kumi kila siku.    

"Watoto wetu wanateseka sana kutembea kwenda shule na wakati mwingine, wengine wanakata tamaa na kuamua kuacha shule kwa umbali" amesema Juliana

Kaimu Mhandisi wa Ujenzi, halmashauri ya Arusha, Mhandisi Bibie Manzi amefafanua kuwa, kiasi hicho cha fedha kitatumika kujenga vyumba sita vya madarasa na meza na viti, ofisi ya walimu na samani za ofisi pamoja na vyoo vya wanafunzi na walimu.

Ameongeza kuwa,  tayari timu ya watalamu imetembea na kukagua eneo la ujenzi na kuandaa michoro na ujenzi huo unategemea kukamilika ndani ya miezi mitano huku taratibu za  ujenzi zikitarajiwa kuanza muda mfupi kuanzia sasa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.