• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KWITEGA AZIKWA KIJIJINI KWAO NGOMA, MAELFU WAMUAGA KWA KUYAENZI MATENDO YAKE

Posted on: February 6th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Maelfu ya waombolezaji waliohudhuri kwenye misa takatifu ya kuaga pamoja na mazishi ya aliyekuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Arusha, marehemu Richard Kwitega, wameyaelezea maisha aliyoishi marehemu Kwitega ni maisha ya ushuhuda kwa wengine, hivyo kifo chake kifanyike funzo kwa maisha ya kila mtu.

Akizungumza wakati wa akitoa salamu zake za pole kwa niaba ya Serikali, Naibu Waziri OR -TAMISEMI, mheshimiwa David Silinde, amesema kuwa maisha aliyoyaishi marehemu Kwitega ni maisha ya ushuhuda wa matendo yanayopaswa kufanywa na mtumishi wa Umma katika kuongoza na kutumikia wananchi, pindi anapoaminiwa na serikali na kupata madaraka ya kuwaongoza wengine pamoja na kuwatumikia wananachi.

"Maisha ya Kwitega yawe funzo kwa kila kiongozi na kila mtu, katika kipindi cha uhai wake na utumishi wake, marehemu Richard aliwekeza katika utu, uzalendo na uadilifu, jambo linalotakiwa kufanywa na kila mtumishi wa Umama aliyepewa madaraka na dhamana ya kuongoza na kuwatumikia wananchi, hivyo viongozi tuliopewa dhamana ya kuwatumikia wengine, tuna wajibu wa kutenda mema kwa wale tunaowatumikia" amesisistiza Naibu Waziri Silinde.

Naye Askofu wa Jimbo la Geita, Mhasham Askofu Flavian Kasala, amemuelezea marehemu Kwitega kuwa, aliishi maisha ya kujitoa kwa ajili ya wengine, na kuthibitisha kuwa ana heri yule anayetenda matendo ya imani, matendo ya kujitoa kwa ajili ya wengine na huu ni ushuhuda wa maisha ya marehemu Kwitega kwa kanisa, jamii na serikali aliyokuwa anaitumikia, katika kipindi chote cha maisha yake ya hapa duniani.

Mkuu wa mkao wa Arusha, Mheshimiwa Idd Kimanta, amesema Serikali imepoteza mtu muhimu, hususani katika mkoa wa Arusha, mtu aliyependa kuwatumikia wananchi, kiongozi aliyetekeleza majukumu yake kwa weledi mkubwa bila kubughi wengine, kiongozi aliyejikita zaidi katika ubobevu wake kwenye masuala ya utawala, kifo cha RAS kiwe fundisho katika utumishi wa umma, Kwitega  ameondoka akiwa na ushuhuda kwa kila mtumishi mkoani Arusha, tupendane, tuheshimiane, tujaliane na zaidi tubebeane matatizo yetu na kuepuka majungu katika sehemu za kazi.

Katibu Tawala wilaya ya Monduli, Robart Siankeni, amesema kuwa, watamuenzi marehemu Kwitega, kwa kuatekeleza yale aliyowaelekeza ikiwa ni pamoja na kusimamia utawala bora na uwajibikaji katika kuwatumikia wananchi, umuhimu wa kutekeleza mipango ya serikali kwa kusimamia miradi ya maendeleo, kubuni vyanzo vya mapato, kuchochea sekta ya utalii katika mkoa wa Arusha, pamoja na kusimamia amani na utulivu, katika maeneo ya kazi.

Meya wa Jiji la Arusha, Maxmiliani Ilagye amesema kuwa, kifo cha Kwitega ni pigo kwa wananchi wa mkoa wa Arusha, tumepoteza mtu mahiri katika utumishi wa umma, na kuwafariji wafiwa kwa kuwaasa kumtegemea Mungu, "Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, hawatatikisika, tumuenzi marehemu Kwitega kwa kumtumaini Bwana, hili ni fundisho la kila mmoja kujitathmini na maisha yake ya hapa duniani.

Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Saad Mtambule, amesema kuwa licha ya kuwa marehemu Kwitega alikuwa kiongozi wa kazi kwa watumishi wa mkoa wa Arusha, la zaidi katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku, hakuwa boss bali alikuwa kiongozi aliyeshirikiana na watumishi wa mkoa wa Arusha kwa kujipambanua kama rafiki, kaka na baba pia.

Naye mwakilishi wa famili ya marehemu Kwitega na Katibu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ngusa Samike, amesema kuwa, familia inamshukuru sana Mungu kwa zawadi ya maisha ya marehemu Richard Kwitega, kwani alikuwa ni kiongozi wa familia, jamii na kuwa maisha yake yote aliishi kwa kuwatumikia watu. 

Marehemu Richard Kwitwega, alifariki kwa ajali ya gari siku ya Jumatano tarehe 03.02.2021, eneo la Mdorii wilaya ya Babati, mkoani Manyara, kwa ajali ya gari, akiwa njiani kuelekea mkoani Dodoma kwa safari ya kikazi.

Marehemu Kwitega amezikwa kijijini kwao, kijiji cha Ngoma kata ya Igalula tarafa ya Nyachenche wilaya ya Sengerema, aidha marehemu Richard Kwitega ameacha Mjane na watoto wanne.

BWANA ALITOA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE!








Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.