• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maafisa Ugani Arumeru, waagizwa kutumia taasisi ya utafiti ya Kilimo TARI kuimarisha kilimo

Posted on: August 31st, 2018

Mkuu wa wilaya ya Arumeru mheshimiwa Jerry Muro amewataka maafisa ugani wa wilaya ya Arumeru kushirikiana kwa karibu na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania 'Tanzania Agricultural Reseach Institute - TARI' kuwezesha wakulima kulima kilimo chenye tija chenye kuzalisha mazao bora.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa rai hiyo,  alipokutana na Mafisa Ugani wa kata 53, kata zinazojumuisha halmashauri mbili za Arusha na Meru wilayani Arumeru, wakati wa kikao kazi, ambacho mheshimiwa Muro amekiita kikao cha mkakati wa kilimo katika wilaya yake, kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano shule ya msingi Green Acress.

Mheshimiwa Muro ameongeza kuwa, licha ya kuwa TARI inahudumia Tanzania nzima lakini  kwa kuwa makao makuu yapo wilayani Arumeru, kuna ulazima wa wilaya ya Arumeru, kuwa eneo la mfano, ambalo  wakulima wataachana na kilimo cha mazoe, na kujikita kwenye kilimo cha kimkakati, kitakachomtoa mkulima kwenye lindi la umasikini kwa kumuwezesha mkulima wa Arumeru kulima kilimo chenye kutumia mbegu bora na kuweza kupata mazao bora.        

"TARI wanafanya tafiti za mbegu za mazao ya hot culture ' kituo kipo Tengeru kwa nini wakulima wetu wasinufaike na kituo hicho? Kuna sababu gani wakulima wangu waendelee kupata hasara kupitia shughuli za kilimo wanazozifanya? Amehoji mheshimiwa Muro  

Aidha amesema kuwa lengo lake, katika kuelekea uchumi wa viwanda ni kuhakikisha wakulima wa Arumeru, wanalima kilimo cha kimkakati chenye kutumia mbegu  bora na kupata mazao bora yenye uwezo wa kuchakatwa na kuongezewa thamani kupitia viwanda vyetu vya ndani na kuuzwa kama bidhaa ghafi na si kuuza mazao kama ilivyozoeleka.

Na kuagiza Maafisa hao kuandaa taarifa itakayoonesha idadi ya wakulima waliopata ujuzi ikiwa na namba zao za simu ili aweze kuwasiliana nao kuthibitisha endapo ni kweli wakulima hao kupata ujuzi huo wa kilimo.

Naye Meneja wa kituo cha utafiti wa kilimo Tanzania -TARI  amesema kuwa, yuko tayari kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa wilaya ya Arumeru, kwa lengo la kuhakikisha wakulima wanalima kimkakati na kuwezesha nchi yetu kuelekea uchumi wa viwanda huku kilimo hicho kikimnufaisha mkulima kwa kumuongezea kipato.

Dkt. Sebastian amefafanua kuwa, taasisi hiyo inatoa huduma kwa watanzania wote ikiwemo wakulima binafsi, taasisi binafsi na za serikali pamoja na makampuni hivyo ni dhahiri kupita watalamu wa taasisi hiyo, wakulima wananafasi kubwa ya kubadili aina ya kilimo na kulima kilimo chenye tija.

Ametaja mazao yanayofanyiwa tafiti ni pamoja na mazao ya mboga, matunda na mazao ya mizizi na kuongeza kuwa, kupita tafiti hizo wamefanikiwa kupata mbegu bora na zinazozalishwa mazao bora.

Hata hivyo Maafisa Ugani hao,  wamempongeza mkuu huyo wa Wilaya, kwa kukaa nao kirafiki na kuwatia moyo juu ya utekelezaji wa majukumj yao,na  zaidi kupanga mikakati  na mipango ya  pamoja, yenye lengo la kuboresha hali ya kilimo kwa manufaa ya wananchi wa Arumeru na taifa kwa ujumla.

Afisa Kilimo kata ya Oloirieni, Justine Ishemwabura, amesema kuwa kikao kazi hicho, kimewapa mwelekeo wa nini cha kufanya ili kuwafikisha wakulima kwenye kilimo chenye tija  

" Nimefurahishwa na kikao hiki, kimsingi kimetupa hamasa ya kufanyakazi, tunaahidi tunakwenda kufanya kazi, kupitia mambo mbalimbali tuliyokumbushana na malengo tuliyojiwekea malengo, ambayo ni rahisi kuyapima baada ya kipindi flani" amesema Afusa Kilimo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.