Na. Elinpa Lupembe.
Kuelekea kuanza zoezi la kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, linalofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, halmashauri ya Arusha kupitia, Jimbo la Uchaguzi la Arumeru Magharibi, wameanza rasmi mchakato wa uboreshaji wa Daftari hilo, kwa kutoa Mafunzo kwa Maafisa Waandikishaji ngazi ya Kata.
Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha na Afisa Mwandikishaji Mkuu Jimbo la Arumeru Magharibi, Dkt. Wilson Mahera, amewataka, Maafisa Waandikishaji hao, ngazi ya kata, kufuatilia kwa umakini mafunzo hayo, yanayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili kuweza kusimamia zoezi hilo kwa uadilifu ndani ya kata zao.
Dkt. Mahera, amewasisitiza kuwa, kazi hiyo ni nyeti na inahitaji umakini na uadilifu wa hali ya juu, ili kutimiza lengo la Serikali la kuandikisha na kuboresha taarifa za wananchi kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi mkuu, unaotegemea kufanyika mwaka ujao 2020.
Amewataja watu wanaotakiwa kujiandikisha ni wananchi wote ambao wamefikisha miaka 18 sasa na wale wanaotegemea kutimiza miaka 18, ifikapo tarehe 28.10.2020, pamoja na kuboresha taarifa za watu ambao wamehama kutoka eneo waliloandikisha mwaka 2015 na kuhamia eneo jingine, watu ambao wamepoteza vitambulisho vyao vya kupigia kura.
Naye Afisa Uchaguzi, Halmashauri ya Arusha, Hadija Mkumbwa, amefafanua kuwa, zoezi hilo linategemea kufanyika kwa muda wa siku 7 tu, kuanzia tarehe 18 -24 Julai, 2019, na kufanyika katika vitongoji vyote vya kata 27, za Jimbo la Arumeru Magharibi, kukiwa na jumla ya vituo 255 vya kujiandikishia.
Hata hivyo mafunzo hayo, yaliambatana na Kiapo cha Kutunza Siri, kilichofanya na Maafisa Waandikishaji ngazi ya kata mbele ya Hakimu Mkazi Mahakama ya Wilaya ya Arusha, Patricia Kisinda.
Hakimu Kisinda, amewapisha Maafisa Waandikishaji hao ngazi ya kata kwa mujibu wa kanuni ya 7(a) ya uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura kwa uchaguzi wa Rais na Wabunge na Kanuni ya 19(a) ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la wapiga kura, Uchaguzi wa Madiwani za mwaka 2018.
Maafisa Uandikishaji ngazi ya Kata Jimbo la Arumeru Magharibi, wakila kiapo cha kutunza siri na kufanyakazi ya Uandikishaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa uadilifu.
Maafisa TEHAMA wakiandaa mashine ya BVR Kit , tayari kwa kutoa mafunzo kwa vitendo kwa Maafisa Uandikishaji ngazi ya Kata, Jimbo la Arumeru Magharibi.
Hakimu Mkazi Patricia Kisinda, Mahaka ya Hakimu Mkazi Arusha akiwaapisha Maafisa Uandikishaji ngazi ya Kata, Jimbo la Arumeru Magharibi kwenye Ukumbi wa Mikutano, Halmashauri ya Arusha.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.