Na. Elinipa Lupembe.
MAAGIZO YA DC ARUMERU KWA WAJUMBE WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI.
"Waheshimiwa Madiwani mnalo jukumu la kuhamasisha wananchi katika maeneo yenu, kushiriki zoezi la Sensa ya Watu na Makazi, itakayofanyika mwakani 2022, hamasisheni wananchi wenu kushiriki zoezi hilo, kwa ajili ya mipango ya maendeleo ya nchi yetu". DC Arumeru - Eng. Ruyango
"Zoezi la utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa kuanzia umri wa miaka 5 - 17, linaendelea katika maeneo yenu, linaratibiwa na Maafisa Elimu Kata, hakikisheni watoto wote wa umri huo wanapata vyeti vya kuzaliwa, kama ilivyo adhma ya Serikali, ili kuondoa changamoto zinazojitokeza mara nyingi kwa vijana ambao hawana vyeti vya kuzaliwa pindi vyeti hivyo vinapohitajika". DC ARUMERU Eng. Richard Ruyango
"Serikali imepokea awamu ya pili ya chanjo ya UVIKO 19, waheshimiwa Madiwani, endeleeni kupambana na ugonjwa huo hatari kwa kuhamasisha wananchi kupata chanjo, viongozi wenzangu kuweni mfano wa kuchanja kama alivyofanya Mhe Rais wetu" DC ARUMERU Eng. Richard Ruyango
"Katika halmashauri yetu tumepokea fedha za mapamabano ya UVIKO 19, kutoka serikali kuu , kiasi cha shilingi Bilioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 100 vya madarasa, vyumba 96 kwa shule za sekondari na madarasa 4 kwa shule mbili za msimgi shikizi, Waheshimiwa Madiwani mnatakiwa kuungana na watalamu wa ngazi zote, kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo katika maeneo yenu, ili iweze kukamilia kwa wakati na viwango vya ubora vinavyolingana na thamani ya fedha" DC ARUMERU -Eng. Richard Ruyango
"Kuna migogoro mingi ya mipaka katika maeneo yetu, kati ya wilaya na wilaya, kata na kata na hata vijiji kwa vijiji, sisi kama viongozi tunapaswa kuungana pamoja, kutatua migogoro hiyo na kupata suluhisho la kudumu, migogoro inatuchelewesha sana kujielekeza kwenye maendeleo, nitoe Rai kwenu ya kuwa na utaratibu wa kutumia watalamu kwa kuzingatia GN za Serikali zilivyoainisha maeneo ya mipaka hiyo" DC ARUMERU Eng. Richard Ruyango
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango (aliyesimama) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Madiwani, kwenye mkutano wa Baraza la Madiwani la kujadili taarifa za robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2021/2022, mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.