• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MADED WAAGIZWA KUFANYA UHAKIKI WA WASTAAFU AMBAO BADO HAWAJALIPWA STAHIKI ZAO

Posted on: December 3rd, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Karibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Prof. Riziki Shemdoe, amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri zote nchini, kufanya uhakiki wa madeni ya waastafu wote, ambao hawajakamilishiwa malipo ya  mafao yao, na kuyawakilisha ofisini kwake, ili serikali iweze kufanya utaratibu wa kuwalipa wastaafu hao.

Katibu Mkuu huyo ameyasema hayo, wakati akizungumza na walimu wa shule tatu za sekondari halmashauri ya Arusha, akiwa kwenye ziara ya kikazi, ya kukagua maendeleo ya ujenzi vyumba 100 vya madarasa, mradi unaotekelezwa kupitia fedha maalum za mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, amepokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya wastaafu kuwa, kuna baadhi yao hwajalipwa mafao yao huku baadhi hawajakamilishiwa baadhi ya stahiki zao, ikiwemo fedha za kusafirisha mizigo, baadhi ya mapunjo ya mishahara yao.

"Ninawaagiza wakurugenzi wote nchini, kufanya uhakiki  kwa wastaafu katika halmashauri zenu, na kubaini wale ambao hawajakamilishiwa malipo yao, ili tujipange namna bora ya kukamilisha malipo yao, serikali inatambua kazi kubwa iliyofanywa na wastaafu hao, kwa kuitumikia nchi katika kipindi chote cha utumishi wao wa Umma, hivyo hatuna budi kahakikisha wanalipwa stahiki zao kwa kuwa ni haki yao" amesisitiza Katibu Mkuu huyo.

Katika ziara hiyo Katibu mkuu huyo, ametembelea shule za sekondari Kiranyi, Mringa na Matevesi na kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba 26 vya madarasa licha ya kuridhishwa na hatua zilizofikiwa, amewataka wasimamizi na watekelzaji wa mradi huo kuongeza kasi kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kwa muda uliopangwa na serikali.


ARUSHA DC

#KaziInaendela✍✍

PICHA ZA MATUKIO YA ZIARA 

Katibu Mkuu OR -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe akitoa maelekezo kwa mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi ( wa kwanza kulia)  mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ghorofa 4 lenye vyumba 13 vya madarasa shule ya sekondari Kiranyi, mradi unaotekelezwa kupitia fedha za Mapambano dhidi ya UVIKO 19


Katibu Mkuu OR -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na walimu wa shuke ya sekondari Kiranyi, mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ghorofa 4 lenye vyumba 13 vya madarasa shuleni hapo, mradi unaotekelezwa kupitia fedha za Mapambano dhidi ya UVIKO 19

Katibu Mkuu OR -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na walimu wa shuke ya sekondari Mringa, mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba 10 vya madarasa shuleni hapo, mradi unaotekelezwa kupitia fedha za Mapambano dhidi ya UVIKO 19


Katibu Mkuu OR -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe katika picha ya pamoja  na walimu wa shuke ya sekondari Kiranyi, mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ghorofa 4 lenye vyumba 13 vya madarasa shuleni hapo, mradi unaotekelezwa kupitia fedha za Mapambano dhidi ya UVIKO 19

Katibu Mkuu OR -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe katika picha ya pamoja  na walimu wa shuke ya sekondari Matevesi,, mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa shuleni hapo, mradi unaotekelezwa kupitia fedha za Mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.