• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAKAMU WA RAIS AWATAKA MADEREVA KUWAHUDUMIA WAJAWAZITO NA WATOTO KWA STAHA...

Posted on: June 23rd, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa Uzinduzi wa Mfumo wa Kurahisisha Usafiri wa Dharura kwa Mama Wajawazito na Watoto wachanga wa M- Mama kwa Mkoa wa Arusha uliofanyika katika Hospitali ya Mount Meru.Tarehe 22 Juni 2023.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa madereva wanaoshiriki katika mfumo wa M- mama kuwahudumia akina mama wajawazito pamoja na watoto kwa staha, huruma na upendo pale wanapowasafirisha kutoka katika maeneo mbalimbali kuelekea katika vituo vya afya.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizindua Mfumo wa Kurahisisha Usafiri wa Dharura kwa Mama Wajawazito na Watoto wachanga wa M- Mama kwa Mkoa wa Arusha katika hafla iliofanyika Hospitali ya Mount Meru leo tarehe 22 Juni 2023.

Aidha ametoa rai kwa wale wote wanaohusika na usajili wa akina mama wajawazito kuhakikisha wanatekeleza jukumu hilo kwa ufasaha na kuzingatia namba ya dharura ya simu (115) inafahamika kwa kubandikwa sehemu mbalimbali ili wananchi waweze kuifahamu kirahisi.

Halikadhalika Makamu wa Rais amesema mfumo wa M-mama utakapoenea nchi nzima utawezesha kutimiza malengo ya kitaifa na kimataifa ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vya watoto wachanga huku akihimiza elimu kuendelea kutolewa kwa wananchi kwa kuwahamasisha wanawake wanahudhuria kliniki muda wote wa ujauzito na kujifungua katika vituo vya kutolea huduma ya afya.

Makamu wa Rais amesema serikali itaendelea kuboresha upatikanaji wa huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga.

Ameongeza kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea na jitihada ya kuongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma za Afya vinavyotoa huduma kamili za dharura na upasuaji ambapo hadi kufikia mwaka 2022 Serikali imeongeza vituo vya Afya zaidi ya 500 kutoka vituo vya Afya 155 mwaka 2017/18 pamoja na kuongezeka vituo vinavyotoa huduma za watoto wachanga (NICU) kutoka 14 mwaka 2018 hadi vituo 165 mwaka 2022.

Vilevile Makamu wa Rais amewasihi wakazi wa Arusha pamoja na mikoa mingine kusajili akina mama wajawazito na kutumia mfumo wa M-mama ili kuwanusuru wao pamoja na watoto.

Amesema mfumo huo ni mkombozi mkubwa kwani kwa mkoa wa Arusha tangu uanze kufanya kazi mwezi Aprili 2023 hadi kufikia tarehe 20 Juni 2023 tayari umeshasafirisha jumla ya dharura 607 ambapo Kati ya hizo, asilimia 82 zilikuwa ni dharura za akina mama na asilimia 18 za watoto wachanga.

Makamu wa Rais amesisitiza kuenezwa nchi nzima, Tanzania Bara na Zanzibar utekelezaji wa mfumo wa M- mama na kuwashukuru wadau wa maendeleo wakiwemo USAID, Vodacom Tanzania Foundation na mshirika wake Vodafone Foundation kwa utekelezaji wa Mfumo huo hapa nchini.

Hadi sasa Mfumo wa Kurahisisha Usafiri wa Dharura kwa Mama Wajawazito na Watoto wachanga wa M- Mama unafanya kazi katika Mikoa 16 ya Tanzania Bara (Shinyanga, Lindi, Mtwara, Morogoro, Dodoma, Manyara, Singida, Simiyu, Mwanza, Mara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Mbeya, Songwe na Rukwa) na Mikoa yote 5 ya Zanzibar.

Aidha, Mikoa mingine 10 ya Tanzania Bara ambayo ni Katavi, Kigoma, Tabora, Iringa, Njombe, Ruvuma, Kagera, Geita, Pwani na Dar es salaam ipo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji wa mfumo huo na inatarajiwa kuanza utekelezaji kabla ya mwezi Oktoba mwaka huu.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.