Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa wadau wa utalii wa vyakula kuwekeza zaidi katika kuandika vitabu vya vyakula vya Kiafrika na machapisho ya kuandaa mapishi ili kuongeza ujuzi na kupunguza woga kwa watalii wa matumizi ya vyakula wasivyovifahamu.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Umoja wa Mataifa wa Utalii wa Vyakula Barani Afrika unaofanyika katika Ukumbi wa Gran Melia Jijini Arusha. Amesema ni muhimu kutangaza kwa kiwango kikubwa vyakula vya kitamaduni vya Afrika ili utalii wa vyakula uweze kukua na kustawi. Ameongeza kwamba kwa sasa watalii wengi hawana ufahamu wa utajiri wa Vyakula vya Kitamaduni vilivyopo Barani Afrika, vilevile ndani ya nchi za Afrika, utalii wa vyakula umewekwa kwa kiwango kidogo katika mikakati ya kitaifa ya maendeleo ya utalii.
Aidha Makamu wa Rais amesema katika kukuza utalii wa vyakula Barani Afrika inahitajika utengaji wa maeneo maalum na njia za kitamaduni ambapo bidhaa za ndani na vyakula vya kipekee vitatayarishwa kwaajili ya watalii kufurahia. Amesema katika njia na vituo hivyo vya chakula, ubora wa vyakula na bidhaa za asili ni lazima kudumishwa. Ameongeza kwamba hivyo kunahitaji ushirikiano wa karibu kati ya wapishi wa vyakula vya asili, wazalishaji wa ndani, waongozaji watalii na wadau wengine wa utalii ili kuhakikisha kuwa huduma zinazotolewa kwa watalii ni endelevu.
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema ipo haja ya kuweka utalii wa vyakula katika msingi wa utambulisho wa utalii wa Afrika ikiwemo kuimarisha mvuto wake kimataifa kwa kuweka mikakati ya kuunganisha uzalishaji wa chakula, uzoefu wa upishi, na huduma za utalii ili kuwa na athari endelevu za ndani za kiuchumi. vyakula vyetu tajiri, kupika na kula kwa ulimwengu.
Kwa upande wa juhudi za ndani ya nchi, Makamu wa Rais amesema katika kuhakikisha kunakuwepo na utalii endelevu wa vyakula, Serikali ya Tanzania imeamua kuimarisha ushirikiano na wazalishaji wa ndani wa kilimo ili kutekeleza mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kuwekeza katika mifumo ya kidijitali inayowezesha uhusiano kati ya watalii, soko pamoja na na wazalishaji halisi wa chakula.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.