Mawakala wa vyama vya Siasa wa Jimbo la Arumeru Magharibi wamekula kiapo cha uadilifu katika majukumu yao kuelekea uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.
Mawakala hao wamekula kiapo mbele ya Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Edna Lukuta hii leo Mei 11,2024 katika shule ya Sekondari Mringa Kwa Kanda ya Ngaramtoni na Kanda ya Mlangarini.
Afisa uchaguzi wa Jimbo la Arumeru Magharibi Ndugu Priscus Silayo akiwataka Mawakala hao kusimamia kiapo chao kwa kutunza siri na uadilifu.
Pia Afisa Mwandikishaji Msaidizi Jimbo la Arumeru Magharibi Ndg Allen Kitutu amesema kiapo hicho kitasaidia kupunguza malalamiko kwa vyama vya siasa hasa katika zoezi la kujiandikisha katika daftari la wapiga kura hivyo mawakala hao watasaidia kutambua wakazi wa maeneo yao husika katika uandikishaji.
Nao Mawakala hao wameahidi kwenda kusimamia kiapo hicho kwa kutenda haki katika zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ambalo linaanza rasmi Mei 16, na kukamilika 22 ,2025 ,
Afisa Uchaguzi Priscus Silayo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili kushiriki zoezi hilo na waweze kushiriki uchaguzi Mkuu kwa kuchagua viongozi bora na wanaotaka.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.