• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MBIO ZA THE GREAT HEALTH RUN ZAFANIKISHA UCHANGIAJI DAMU SALAMA ARUSHA DC

Posted on: July 28th, 2022

Na Elinipa Lupembe - ARUSHA.

Mbio za maalumu za Kilomita 10 zilizokwenda kwa jina la The Great Health Run, zilizofanyi katika halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, zimefanikisha dhamira ya uchangiaji Damu Salama, ili kuokoa maisha.

Mbio hizo zilizoambatana na zoezi la uchangiaji damu Salama, na kufanikisha kupata uniti 10 za damu, pamoja na ugawaji wa vifaa vya kupimia uzito kwa watoto kwenye vituo vitano vya afya vya halmashauri hiyo.

Mgeni rasmi katika mbio hizo, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amewapongeza waandaji na washiriki wa mbio hizo na kuwataka wananchi kuona umuhimu wa kujitoa kuchangia damu, kwa kuwa uwepo wa damu ya akiba, husaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wa dharura katika hospitali nchini.

Aidha ametoa wito wa wananchi kufanya mazoezi binafsi pamoja na kushiriki mbio zinazoandaliwa na wadau mbalimbali, kwa kuwa licha ya kuimarisha afya ya mwili, mazoezi huzuia magonjwa mengi yasiambukiza kama kisukari, uzito uliokithiri pamoja na shinikizo la damu.

"Inafahanika kuwa siri kubwa ya kufanya mazoezi, ni kuimarisha mwili na kuufanya kuwa 'active', mazoezi yanamfanya mtu kuwa kama kijana, kuna wazee wenye zaidi ya miaka 65, tumekiambia nao na ukiwatizama afya zao utadhani vijana, hii ni kutokana na kufanya mazoezi".Amesisitiza Mkurugenzi Msumi

Aidha Mkurugenzi Msumi, amewashukuru watu wote waliojitoa kuchangia damu na kusistiza jamii umuhimu wa kuchangia damu ni pamoja na kuokoa maisha ya watu hususani wagonjwa wa dharura, hivyo kuwa na tabia ya kuchangia damu kila inapobidi.

Naye Kaimu Mganga Mkuu, halmashauri ya Arusha, Dkt. Japhet Champanda amekiri uwepo wa uhitaji wa Damu katika vituo vya kutolea huduma za afya, unaolazimu  kuwa na akiba ya damu katika hospitali, na kutumika pindi wanapotokea wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu.

"Tunauhitaji wa damu usiopungua  uniti 100 kwa mwezi na uniti 1,200, kwa mwaka, utaona namna uhitaji wa damu ulivyo mkubwa, damu ambayo hutumika zaidi kwa kina mama wakati wa kujifungua, wagonjwa dharura na majeruhi wa ajali". Amefafanua Dkt. Champanda.

Hata hivyo, Dkt. Champanda ameeleza umuhimu wa kufanya mazoezi ya viungo mara kwa mara, kuwa inapunguza magonjwa yasiyo ya lazima, na kusisistiza pamoja na kuzingatia mazoezi, watu wanatakiwa kuzingatia ulaji wa vyakula vyenye lishe bora.

Awali muandaaji wa mbio hizo na Muuguzi wa Zahanati ya Moivo Kilie Ghubi, amesema kuwa mbio hizo zenye lengo la kuchangia damu kuokoa maisha, zimeambatana
na ugawaji wa vifaa vya kupima uwiano wa uzito, urefu na umri kwa watoto wachanga (stadiomita), vifaa vilivyogawiwa kwenye vituo vitano vya afya, halmashauri ya Arusha.

 Ghubi amewashukuru watu wote waliojitokeza kushiriki mbio hizo, sambamba na uchangiaji wa damu salama, na kubainisha kuwa jumla ya watu 756 wameshiriki mbio hizo.

SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI 23.AUGUST 2022
JIANDAE KUHESABIWA✍✍✍



PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MBIO ZA THE GREAT HEALTH FUN



Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi (wa pili kushoto) akizungumza wakati wa kuhitimisha Marathon ya The Great Health Run kwenye viwanja vya makao Makuu ya Halmashauri ya Arusha.






Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi,


Muandaaji wa Mbio za The Great Health Run, Kilie Ghubi (Kulia) akimkabidhi keki, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, wakati wa kuhitimisha  mbio hizo, kwenye viwanja vya makao Makuu ya Halmashauri ya Arusha.



Mwenyekiti Halmashauri ya Arusha, mhe. Ojung'u Salekwa akimlisha keki mtoa huduma kutoka Kivulini Martenity, wakati wa kuhitimisha Marathon ya The Great Health Run kwenye viwanja vya makao Makuu ya Halmashauri ya Arusha.


 Wahirikim wa Marathon ya The Great Health Run wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi (wa pili kulia)  wakati wa kuhitimisha zoezi hilo kwenye viwanja vya makao Makuu ya Halmashauri ya Arusha.



SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI 23, August 2022

JIANDAE KUHESABIWA ✍✍

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.