Na Elinipa Lupembe.
Victor Karia mdau, mkazi na mjumbe wa kamati ya Afya Halmashauri ya Arusha, akiwasilisha mada juu Mapambano dhidi ya maradhi katika ustawi na maendeleo ya jamii tangu kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.
Bw. Karia amezungumzia hali halisi ya mabadiliko katika sekta ya afya kuanzi mtu binafsi, upatikanaji wa huduma za afya, uwezeshwaji wa jamii kupata huduma za afya pamoja na ushirikishwaji wa jamii katika kupambana na magonjwa kupitia watoa huduma ngazi ya jamii.
Bw. Karia amebainisha mabadiliko ya kiafya yaliyotokana na mapambano ya ujinga na kumuwrzesha mtanzania mwenyewe kufahamu namna ya kujikinga na maradhi kupitia lishe bora na usafi wa mtu na mazingira,jambo ambalo zamani watu wengi walipoteza maisha kutokana na magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu, surua, utapiamlo magonjwa ambayo watanzania wa sasa wamefahamu namna ya kujikinga.
Serikali imefanikiwa kuboresha sekta ya afya kwa kusogeza huduma za afya, karibu na wananchi kwa kuhakikusha kila kijiji kina zahanati, kata ina kituo cha afya, hosptali ya wilaya na kuwa hosptali za rufaa za mkoa, jambo ambalo licha ya kurahisisha upatikanaji wa matibabu, limeondoa msongamano hospitalini.
"Tulikotoka tilitegemea hospitali 1 ya rufaa ya Muhimbili, lakini kwa sasa hospitali za rufaa zipo nyingi, hii ni zao la uwepo wa watalam wasomi na wazawa, waliozalishwa ndani ya nchi yetu".Amfafanua Karia
Mdahalo uliojumisha wananchi wa makundi na rika tofauti wa halmashauri ya Arusha ulijikita kujadili mada ya "MIAKA 61 YA UHURU NA MAPAMBANO DHIDI YA MAADUI UJINGA, UMASKINI NA MARADHI", uliongozwa na Katibu Tawala Wilaya ya Arumeru Mwl. James Mchembe, uliofanyika kwenye ukumbi wa shule ya Msingi Green Acres eneo la Sekei.
Mdahalo ni maalum kuelekea maadhimisho ya sikuu ya Uhuru wa Tanganyika tarehe 09.12.2022.
MIAKA 61 YA UHURU "Umoja na Amani ndio nguzo ya watanzania wote "
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
Bw. Victor Karia akiwasilisha mada juu Mapambano dhidi ya adui maradhi kwenye Mdahalo wa kuelekea Miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika, uliofanyika kwenye Ukumbi wa shule ya Msingi Green Acres.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.