• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MSAHIKI MEYA WA JIJI LA ARUSHA Mhe.MAXIMILIAN AWA MWENYEKITI WA ALAT MKOA WA ARUSHA.

Posted on: April 15th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Msahiki Meya wa Jiji la Arusha Mheshimiwa Maximilian Iranghe, amekuwa  Mwenyekiti wa Jumuia ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanzania - ALAT mkoa wa Arusha, mara baada ya kuibuka kidedea kwa kumshinda mpinzani wake, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Monduli, kwenye uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, aliyekuwa Mwenyekiti wa muda wa  kikao hicho na Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Ojung'u Salekwa, amesema kuwa katika uchaguzi huo, mheshimiwa Maximilian Iranghe amepata kura 15  kati ya kura 28 zilizopigwa na kumshinda mpinzani wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Monduli, mheshimiwa Isack Capricorn  aliyepata kura 13.

"Kwa Mamlaka niliyopewa, kwa mujibu wa sheria na kanuni za serikali za mitaa,  na kutokana na  matokeo hayo kura zilizopigwa, ninamtangaza Meya wa Jiji la Arusha, mheshimiwa Maximilian Iranghe kuwa Mwenyekiti wa ALAT mkoa wa Arusha, na kuiongoza jumuia hiyo kwa kipindi cha miaka mitano" ametangaza Mheshimiwa Salekwa.

Akizungumza baada ya kutangazwa, Mwenyekiti mpya wa ALAT mkoa wa Arusha, mheshimiwa Maximilian Iranghe, licha ya kuwashukuru wajumbe kwa kumuamini na kumchagua, amewataka kufanyakazi kwa kushirikiana kama timu, imani ambayo anaamini itawezesha kufikia lengo moja la kuwatumikia wananchi wa mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla.

"Ninaamini katika kufanyakazi kwa kushirikiana pamoja, nanukuu usemi usemao 'ukitaka kufika haraka nenda peke yako, lakini ukitaka kufika mbali nenda na wenzako', kama viongozi na wawakilishi wa wananchi lengo letu ni kuitoa ALAT hapa ilipo na kuipeleka mbali zaidi kufuatia malengo na mipango ya tuliyojiwekea kwa maslahi ya wananchi na  taifa letu la Tanzania "amesisitiza Mwenyekiti huyo mpya wa ALAT mkoa wa Arusha.

Hata hivyo katika uchaguzi huo, nafasi ya Makamu mwenyekiti, imechukuliwa na  mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Ojung'u Salekwa, huku nafasi ya Katibu ikichukuliwa na mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya wilaya ya Karatu, wakati nafasi ya mbunge mwakilishi ALAT mkoa, ikichukuliwa na Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, mheshimiwa Noah Lembris.

Aidha katika mkutano huo, kikanuni wajumbe waliwachagua wajumbe watano wa Kamati tendaji, ambapo mhe. Glory Kaaya  Diwani mwakilishi, halmashauri ya Meru, Mhe.Isaya Doita, Diwani mwakilishi  halmashauri ya Jiji la Arusha, Mhe. John Mahuu, Mwenyekiti wa halmashauri ya Karatu, Mhe. Miryam Kissamike Diwani mwakilishi Jiji la Arusha, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Monduli, Steven Ulaya.

Jumuia ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanzania katika ngazi ya mkoa, inayoundwa na mameya wa majiji,  wenyeviti na wakurugenzi wa halmashauri, wabunge wa majimbo yote pamoja na madiwani wawakilishi wawili kutoka katika halmashauri saba za mkoa wa Arusha.







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.