• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MHE. RAIS SAMIA AWAAHIDI MAJI WANANCHI WA KISONGO

Posted on: November 28th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewaahidi wananchi wa Kisongo kuwasiliana na Wizara ya maji kuona namna ya kuunganisha  mradi wa maji wa bilioni 600 wa Jiji la Arusha ili kuwafikia wananchi hao.

Mhe. Rais ameyasema hayo kwenye Mkutano wa Hadhara, uliofanyika kwenye soko la Kisongo kata ya Mateves, Halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, wakati akiwaaga wananchi wa mkoa wa Arusha mara baada ya kumaliza ziara yake mkoani humo.

"Tumemaliza tatizo la maji Jiji la Arusha kupitia mradi wa maji wa Bilioni 600, mahitaji ya Jiji la Arusha ni lita milioni  90 tu, na maji hayo yamezidi, tutafanya mpango kuhakikisha maji hayo yanaunganishwa hapa, ili wananchi wa Kisongo mpate maji, Kisongo maji yatapatikana". Amesema Mhe. Rais

Mhe. Rais amewahakikishia wana Kisongo maji na kuongeza kuwa Wizra ya maji inatekeleza miradi mingi kwa sasa, ikitokea bakaa yoyote ipelekwe Arumeru ili kumaliza tatizo hilo.

Katika mkutano huo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Mhe. Noah Lembris alipata fursa ya kuwasilisha changamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo hilo ikiwemo miundombinu ya barabara za ndani, maji, ujezni wa soko la Kisongo pamoja na mpaka wa mita 200 kati ya Arusha DC na Jiji la Arusha.

Aidha Mbunge huyo licha ya kuwasilisha changamoto hizo amemshukuru na kumpongeza Mhe. Rais kwa serikali kutoa fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo jimboni humo.

"Kupitia TARURA tumepokea bilioni 1.5 za ujenzi wa barabara za ndani, umesaini mkataba wa bilioni 22 za ujenzi wa barabara ya lami Km 18 Mianzini, Timbolo- Ngaramtoni, milioni bilioni 1,4 za kukamilisha vituo vya afya, milioni 450 kumaliza zahanati 11 lakini pia tumepokea milioni 760 za ujenzi wa madarasa 38 shule 15 za sekondari kwa ajili ya wanafunzi wankidato cha kwanza 2023". Amebainisha Mhe. Noah.

Hata hivyo Katibu Mkuu TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe ameitaja mikakati ya ujenzi wa barabara za ndani katika halmashauri hiyo na kusema kuwa serikali itazingatia mahitaji yaliyowasilishwa na kuweka kwenye mpango wa bajeti kwa mwaka ujao wa fedha.

"Ujenzi wa soko ni mradi mkakati, nitamuelekeza Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha, kuandika andiko likikidhi vigezo, tutakaa na Wizara ya fedha ili mrafi huu uanze". Amesema Katibu mKuu huyo.

Hata hivyo Mhe. Rais ametumia fursa hiyo kuwaaga wananchi wa Arusha na kuweka wazi kuwa atarudi Arusha kwa kuwa, Arusha ni kiini cha shughuli za za Serikali na mataifa ya nje.

Awali, Mhe.  Rais amefanya mkutano huo akiwa njiani kurejea jijini Dodoma mara baada ya kumaliza ziara ya siku 4 ya kikazi Mkoani Arusha.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍







Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA NAFASI ZA UDEREVA TAREHE 28/12/2018 December 19, 2018
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI TAREHE 1-7, AGOSTI 2020. July 31, 2020
  • TANGAZO KWA WANANCHI WOTE MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA PILI 2O20/2021 TAREHE 29.01.2021 January 29, 2021
  • KINGA TIBA YA KICHOCHO NA MINYOO YA TUMBO KWA WATOTO MIAKA 5-14 March 02, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • BALOZI WA JAPAN NCHINI AMEKABIDHI MTAMBO WA KICHUJIA MAJI KUONDOA MADINI YA FLORAIDE KIJIJI CHA LEMANDA

    January 28, 2023
  • BALOZI WA JAPAN NCHINI AMEKABIDHI MTAMBO WA KICHUJIA MAJI KUONDOA MADINI YA FLORAIDE KIJIJI CHA LEMANDA

    January 28, 2023
  • MWENYEKITI ARUSHA DC MHE. OJUNG'U SALEKWA AKIPANDA MTI ENEO LA MTAMBO WA KUCHUJIA MAJINKIJIJI CHA LEMANDA

    January 27, 2023
  • BALOZI WA JAPAN NCHINI TANZANIA AZINDUA MTAMBO WA KUCHUJIA MAJI KIJIJI CHA LEMANDA....

    January 27, 2023
  • Tazama zote

Video

MFUGAJI AKIELEZEA FAIDA ZA UHIMILISHAJI WA NG'OMBE WA MAZIWA - BANDA LA MIFUGO ARUSHA DC
Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.