Na Elinipa Lupembe
Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewaahidi wananchi wa Kisongo kuwasiliana na Wizara ya maji kuona namna ya kuunganisha mradi wa maji wa bilioni 600 wa Jiji la Arusha ili kuwafikia wananchi hao.
Mhe. Rais ameyasema hayo kwenye Mkutano wa Hadhara, uliofanyika kwenye soko la Kisongo kata ya Mateves, Halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, wakati akiwaaga wananchi wa mkoa wa Arusha mara baada ya kumaliza ziara yake mkoani humo.
"Tumemaliza tatizo la maji Jiji la Arusha kupitia mradi wa maji wa Bilioni 600, mahitaji ya Jiji la Arusha ni lita milioni 90 tu, na maji hayo yamezidi, tutafanya mpango kuhakikisha maji hayo yanaunganishwa hapa, ili wananchi wa Kisongo mpate maji, Kisongo maji yatapatikana". Amesema Mhe. Rais
Mhe. Rais amewahakikishia wana Kisongo maji na kuongeza kuwa Wizra ya maji inatekeleza miradi mingi kwa sasa, ikitokea bakaa yoyote ipelekwe Arumeru ili kumaliza tatizo hilo.
Katika mkutano huo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Mhe. Noah Lembris alipata fursa ya kuwasilisha changamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo hilo ikiwemo miundombinu ya barabara za ndani, maji, ujezni wa soko la Kisongo pamoja na mpaka wa mita 200 kati ya Arusha DC na Jiji la Arusha.
Aidha Mbunge huyo licha ya kuwasilisha changamoto hizo amemshukuru na kumpongeza Mhe. Rais kwa serikali kutoa fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo jimboni humo.
"Kupitia TARURA tumepokea bilioni 1.5 za ujenzi wa barabara za ndani, umesaini mkataba wa bilioni 22 za ujenzi wa barabara ya lami Km 18 Mianzini, Timbolo- Ngaramtoni, milioni bilioni 1,4 za kukamilisha vituo vya afya, milioni 450 kumaliza zahanati 11 lakini pia tumepokea milioni 760 za ujenzi wa madarasa 38 shule 15 za sekondari kwa ajili ya wanafunzi wankidato cha kwanza 2023". Amebainisha Mhe. Noah.
Hata hivyo Katibu Mkuu TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe ameitaja mikakati ya ujenzi wa barabara za ndani katika halmashauri hiyo na kusema kuwa serikali itazingatia mahitaji yaliyowasilishwa na kuweka kwenye mpango wa bajeti kwa mwaka ujao wa fedha.
"Ujenzi wa soko ni mradi mkakati, nitamuelekeza Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha, kuandika andiko likikidhi vigezo, tutakaa na Wizara ya fedha ili mrafi huu uanze". Amesema Katibu mKuu huyo.
Hata hivyo Mhe. Rais ametumia fursa hiyo kuwaaga wananchi wa Arusha na kuweka wazi kuwa atarudi Arusha kwa kuwa, Arusha ni kiini cha shughuli za za Serikali na mataifa ya nje.
Awali, Mhe. Rais amefanya mkutano huo akiwa njiani kurejea jijini Dodoma mara baada ya kumaliza ziara ya siku 4 ya kikazi Mkoani Arusha.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.