Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Nembo ya Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 na kutangaza rasmi zoezi la Sensa kufanyika tarehe 23.Agosti 2022.
Mheshimiwa Rais amesisistiza kuwa, ni jukumu la kila mtanzania kishiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya watu na makazi.
Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), imekamilisha maandalizi ya kufanya Sensa hiyo.
Ifahamike kiwa, Sensa ya Watu na Makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka 10 ambapo Sensa ya mwisho kufanyika nchini ni ile ya mwaka 2012.
Sensa ya mwaka 2022 itakuwa ni sensa ya Sita kufanyika nchini baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, 2002 na 2012.
"JIANDAE KUHESABIWA"
ARUSHA DC
KaziIendelee ✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.