• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MILIONI 200 ZA PROGRAM YA P4R ZAJENGA ZAHANATI KIJIJI CHA MUSA - ARUSHA DC

Posted on: June 12th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

     Serikali kipitia programu ya lipa kutokana na matokeo (P4R), imetoa kiasi cha shilingi milioni 200,  kukamilisha na kupanua ujenzi wa miundombinu ya zahanati ya kijiji cha Musa, kata ya Musa, halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, jengo ambalo lilianza kujengwa kwa nguvu za wananchi wa kijiji hicho.

      Lengo la mradi huo likiwa ni utekelezaji mkakati wa serikali ya awamu ya tano wa kuhakikisha, huduma muhimu za afya zinawafikia wananchi katika maeneo yao, kwa kila kijiji kuwa na zahanati, kata kuwa na kituo cha afya, wilaya kuwa na hospitali ya wilaya kadhalika kila mkoa kuwa na haspitali ya Rufaa, jambo ambalo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

       Mganga mkuu halmashauri ya Arusha Dkt. Peter Mboye, ameeleza kuwa mradi huo ni muhimu kwa wananchi wa kijiji cha Musa na vitongoji vyake, licha ya uchakavu wa jengo la zahanati iliyokuwepo kuendelea kutoa huduma, lakini pia jengo hilo lilikuwa dogo, lisilokidhi mahitaji,  kulinganisha na idadi ya wateja wanaohudumiwa katika zahanati hiyo kwa siku.

     Dkt. Mboye amefafanua kuwa, kiasi hicho cha fedha kimetumika kumalizia jengo la zahanati ambalo lilianzwa kujengwa na wananchi, jengo ambalo limebeba sehemu ya wagonjwa nje 'OPD', maabara, kliniki ya mama na mtoto, nyumba ya daktari pamoja na vyoo vya nje, ujenzi ambao unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu wa 2020.

       Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Musa, Ernest Lesikari, pamoja na kuishukuru serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli, amethibitisha umuhimu wa mradi huo kwa wananchi,  si wa kijiji cha Musa pekee yao, bali na wananchi wa vijiji jirani vya kata nzima ya Musa.

        "Jengo la zahanati lililopo, lilijengwa miaka mingi iliyopita,  kukiwa na idadi ndogo ya watu, lakini tayari limechakaa, na halitoshi kuhudumia wagonjwa wengi kulingana na idadi kubwa ya  wagonjwa waofika zahanati hapo kupata huduma kila siku "amesema Mwenyekiti huyo.

     Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa, tangu serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani, hali ya upatikanaji wa huduma za afya katika zahanati hiyo zimeimarika kwa kiasi kikubwa, ikiwemo upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, huduma za kujifungua kwa wajawazito, kliniki ya mama na mtoto pamoja  na huduma zote muhimu tofauti na miaka ya nyuma.

   Namnyaki Matayo, mkazi wa kijiji cha Musa, amesema kuwa, ujenzi wa zahanati hiyo, umeleta matumaini makubwa kwa wanawake wa kijiji hicho, kwa kuwa wao ndio walezi wa familia, ambao mara nyingi, huteseka wakati wa kujifungua na kuhudumia wagonjwa ndani ya familia zao.

      "Kina mama ndio hupata mateso hasa wakati wa kujifungua, na sisi ndio tunakimbizana na wagonjwa wa familia, mara hospitali ya Monduli, Olturumeti lakini sasa tuna nerma tunapata huduma bora hapa karibu, kina mama tutapumzika sasa" amesema Namnyaki

      Awali ujenzi wa Zahanati hiyo, umeanza mwezi wa Machi na unategemea kukamilika mwishoni mwa mwezi huu wa Juni na kuanza kutoa huduma kwa wananchi wa kata ya Musa na Vitongoji vyake.


PICHA ZA MAJENGO YA ZAHANATI HIYO










Msingi wa nyumba ya Daktari.

Jengo la zahanati ya zamani kijiji cha Musa

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.