Na Elinipa Lupembe
Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF imetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 350 kwa ajili ya ujenzi wa kituo kipya cha afya kata ya Bwawani, mradi ambao utatekelezwa kwa kipindi cha miezi 12 kwa mwaka wa fedha 2023/20224.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi amesema kuwa, tayari utekelzaji wa mradi huo umeanza kwa kasi huku wananchi wa kata ya Bwawani na vijiji vyake wakishiriki katika ujenzi huo.
Ameongeza kuwa ujenzi wa kituo hicho cha afya umekuja wakati muhimu sana, kutokana na adha kubwa walioyokuwa wakiipata wanachi wa kata hiyo kwa kukosa huduma za afya kwa magonjwa ambayo huduma zake kushindikana kwenye zahanati.
"Kukamilika kwa mradi huu kutoandoa changamoto za vifo vya kina mama na watoto, wakati wa kujifungua lakini zaidi kinategemea kuhudumia watu zaidi ya elfu 18 ikiwemo watu elfu 12 wa kata ya Bwawani na takribani watu elfu 6 wa kata za jirani za halmashauri ya Meru na Simanjiro mkoani Manyara" Amebainisha Mkurugenzi Msumi.
Naye mratibu wa TASAF halmashauri ya Arusha Grace Makema, amesema kuwa kiasi hicho cha fedha kitatumika kujenga majengo matatu ikiwemo jengo la wagonjwa wa nje (OPD), Jengo la mama na mtoto ( maternity ward) pamoja na nyumba ya watumishi (3in 1).
Ikumbukwe kuwa lengo la serikali ni kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati na kila kata inakuwa na kituo cha afya huku kila wilaya ikiwa na hospitali ya wilaya pamoja na hospitari za rufaa za mkoa kwa kila mkoa.
ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA
#kaziiendelee
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.