• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Milioni 480 tena, Arusha DC kujenga na kukarabati miundombinu ya elimu

Posted on: April 26th, 2018

Halmashauri ya Arusha imeanza ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu, baada ya serikali kuongeza fedha nyingine kiasi cha sh milioni 480, fedha za mradi wa lipa kutokana na matokeo (Payment for Result 'P4R').

Fedha hizo zimekuja mara baada ya halmashauri hiyo, kukamilisha kwa umakini na kwa wakati, mradi wa awali wa P4R wenye thamani ya shilingi milioni 500.

Kiasi hicho cha fedha cha shilingi milioni 480, kimetolewa  kwa ajili ya ujenzi na ukarabati miundo mbinu ya shule kufuatia adhma ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa na shule zenye miundombinu na mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia.  

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, wakati akikagua maendeleo ya miradi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera amekiri kupokea kiasi  cha shilingi milioni 480 na kueleza kuwa fedha hizo zinatumika kwa shule za msingi na sekondari kwa mgawanyo unaokaribiana.

Dkt. Mahera amefafanua mgawanyo wa fedha hizo kuwa, kiasi cha shilingi milioni 227 zitatumika kwa shule za msingi,  ambapo milioni 96 zinatumika kujenga vyumba vinne vya madarasa, kwa gharama ya shilingi milioni 24 kwa kila darasa pamoja na kununua madawati katika madarasa hayo.

Aidha shilingi milioni 96 nyingine zitatumika kusawazisha ikama ya walimu na milioni 35  zitatumika katika ukusanyaji wa takwimu muhimu za shule zote za msingi, takwimu zitakazosaidia kupata picha halisi ya hali ya shule, wanafunzi na uendeshaji wa shule wenye lengo la kuendelea kufanya maboresho katika suala zima la elimu shuleni.  

Ameendelea kueleza kuwa kiasi kingine cha shilingi milioni 253 kinatumika kukarabati na kumalizia miundombinu ya maabara za sayansi kwenye jumla ya shule 7 za sekondari pamoja na kujenga vyumba 5 vya madarasa kwenye shule nne za sekondari.  

Aidha Dkt. Mahera amethibitisha kuwa, miradi yote imeanza kutekelezwa kwa kasi kwenye shule zote zilizoainishwa na kuongeza kuwa, kukamilika kwa miundombinu hiyo ya shule, kutaongeza ufanisi na ari ya wanafunzi kujifunza na walimu kufundisha, jambo ambalo anaamini litapandisha kiwango cha taaluma katika  shule hizo.

Naye Afisa Elimu Sekondari, halmashauri ya Arusha, mwalimu Sofia Msofe amesema kuwa, kukamilika kwa maabara katika shule za sekondari kutaleta tija na hamasa kwa wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi kutokana kujifunza kwa nadharia na vitendo pia.    

 "Mimi ni mwalimu wa Biolojia, masomo ya  Sayansi bila kufanya kwa vitendo ni kubahatisha, lakini once mwanafunzi akijifunza kwa nadharia akafanya kwa vitendo ni rahisi kuelewa na kukumbuka, na zaidi kulipenda somo" amesema Afisa Elimu huyo.  

Nakuongeza kuwa awali masomo ya Sayansi yalikuwa yanafundishwa kwa kufanya 'alternative to practical' jambo ambalo wanafunzi walikuwa wanalazimika kukariri zaidi bila kuelewa, lakini uwepo wa maabara, wanafunzi sasa watafanya kwa vitendo na kwa uhalisia zaidi jambo ambalo licha ya kuongeza uwelewa wanafunzi pia hufurahia somo.

Awali fedha za P4R kiasi cha shilingi milioni 500, zilitumika kujenga vyumba 8 vya madarasa ya kidato cha 5&6, ukarabati wa maabara za sayansi, mabweni ya wasichana na vyoo kwenye shule za sekondari Mlangarini na Mwandeti, mradi ambao ulikamilika kwa wakati na tayari  wanafunzi wanafaidika na matunda ya mradi huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.