Na Elinipa Lupembe
Mahakam ya Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha imemhukumu kifungo cha miaka 30 na kifungo cha maisha jela, Bw. Fadhili Sumaiyani mwenye umri wa miaka 30, mkazi wa Kitongoji cha Seuri, Kata ya Olturumet halmashauri ya Arusha kwa kosa la kumbaka na kumlawiti mtoto wa miaka tisa.
Akitoa hukumu hiyo Julai 19, 2022 Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya wilaya, Gwantwa Mwankunga, amesema kuwa, Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo, mara baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa pasipo na shaka yoyote na kumtia hatiani mtuhumiwa huyo kwa makosa mawili la kubaka na kulawiti.
Hakimu huyo amemtianhatiani kwa kosa la kubaka chini ya kifungu na 154 na kosa la kubaka chini ya kifungu cha 130 na 131 vya kanunia ya adhabu.
Mwendesha mashitaka na Wakili wa Serikali Liliani Mmasi, aliieleza mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 19 Mei, 2021 katika Kitongoji cha Seuri, kwenye eneo analofanyia kazi ya ulinzi mtuhumiwa, ambapo alimbaka na kumlawiti mtoto huyo wa miaka tisa mwanafunzi wa darasa la tatu, na kumsababishia maumivu makali.
Muendesha mashtaka huyo, amefafanua kuwa, mtuhumiwa alimbaka na kumlawiti mtoto huyo majira ya saa 11 jioni, wakati mtoto huyo akielekea dukani, alikokuwa ametumwa na mama yake kununua mahitaji ya nyumbani, katika eneo ambalo mtuhumiwa anafanya kazi ya kulinda nyumba ambayo haijakamilika ujenzi.
Aidha Mwendesha mashitaka, aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mtuhumiwa kwa makosa yote mawili, ili iwe ni fundisho kwa watu wengine wenye nia ovu ya kutaka kufanya vitendo kama hivyo kwa watoto.
Upande huo wa mashitaka uliwasilisha mashahidi watano ambao pasipo kuacha shaka yoyote mahakama ilimkuta mtuhumiwa na makosa mawili, na kuamua kumtia hatiani kwa kumfunga kifungo cha miaka thelathini kwa kosa la kubaka na kifungo cha maisha kwa kosa la kulawiti, na kutumikia adhabu zote mbili kwa pamoja huku adhabu kubwa ikibeba adhabu ndogo.
Awali mkurugenzi wa shirika la lisilo la kiserikali CWCD, Hindu Mbwega, ameishukuru mahakama kwa kumtia hatiani mtuhumiwa huyo, kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukatili kwa watoto, na kuionya kuacha kufanya vitendo hivyo huku akiitaka jamii kuwafichua watu wanaofanya vitendo vya ukatili kwa watoto na kuwasisitiza watu wenye nia ovu kutambua kuwa sheria inafanya kazi kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo hivyo.
Naye Afisa Ustawi wa Jamii, halmashauri ya Arusha, Josina Mlaki ameweka wazi kuwa, licha ya kuwa serikali kwa kushirikiana na ASAS za kiraia wanatoa elimu kwa jamii juu haki za mtoto pamoja na kumlinda mtoto dhidi ya vitendo vya ukatili lakini bado kuna changamoto ya jamii kukosesha watoto haki zao, kwa kukataa kutoa ushahidi na kusababisha baadhi ya kesi kushindwa kuwatia hatiani watuhumiwa huku wakiwa wamefanya makosa hayo kwa watoto.
Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 75 ya vitendo vya ukatili kwa watoto nchini, vinafanywa na watu wa karibu ndani ya familia na jamii zinazowazunguka watoto.
ARUSHA DC
KaziIendelee✍✍
JIANDAE KUHESABIWA
Bw. Fadhili Sumaiyani mwenye umri wa miaka 30, mkazi wa Kitongoji cha Seuri, Kata ya Olturumet halmasahuri ya Arusha amehukumiwa kifungo cha maisha kwa kosa la kumbaka na kumlawiti mtoto wa miaka tisa.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.