Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Arusha,Bwana Suleiman Msumi leo tarehe 23/01/2025 amekutana na kufanya mazungumzo wawakilishi wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation toka Nchini Marekani.
Lengo la ziara ya Taasisi hiyo ya Bill & Melinda Gates Foundation ni kufanya tafiti za mazao ya Kilimo kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania ( TARI-SERIAN) kwenye Halmashauri ya Arusha kwa kubainisha changamoto zinazowakabili wakulima na kuona namna bora ya kuzitafutia ufumbuzi.
Baadhi ya changamoto zilizoainishwa kwa wakulima katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha ni pamoja na uzalishaji duni wa mazao ya kilimo, wakulima kukosa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea,Viuatilifu, mbegu pamoja na changamoto za mabadilko ya Tabia Chini.
Kwa upande wake,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha bw.Suleiman Msumi amewashukuru na kuwahakikishia wageni hao toka Taasisi ya Melinda and Bill Gates Marekani kwa kuichagua Halmashauri ya Arusha kutekeleza miradi ya utafiti ambayo itasaidia na kuongeza ufanisi katika kuzalisha mazao ya kilimo.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.