Na Angela Msimbira, ZANZIBAR
Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman amezindua Mpango wa Uwekezaji wa Afya ya Mama na Mtoto Tanzania wa miaka mitano (Tanzania Martenal & Child Health Investment Program) wenye lengo la kuimarisha afya ya Mama na mtoto nchini unaofadhiliwa na Benki ya Dunia pamoja na Shirika la Global Financing Facility.
Akizundua Mpango huo leo Agosti 23,2022 Zanzibar .Mhe Othman amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi kwa kuendelea kutoa kipaombele katika sekta ya afya na kuwezesha uzinduzi wa mpango wa uwekezaji katika afya ya mama na mtoto unaolenga kuboresha huduma ya afya ya mama na mtoto katika ngazi zote Tanzania Bara na Zanzibar.
Amesema Mpango huo utatekelezwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya Tanzania Bara, Wizara ya Afya Zanzibar pamoja na Ofisi ya Rais TAMISEMI ambapo uwekezaji wake utagharimu dola za Marekani milioni 275 na kati ya hizo dola za Marekani 250 ni mkopo wa gharama nafuu kutoka Benki ya Dunia na dola za Marekani milioni 25 kutoka Global financing facility.
Mhe. Othman amesema kuwa, kwa upande wa Tanzania Bara Mpango huu utatekeleza afua muhimu ikiwemo kuajiri watumishi 1, 000 wa kada mbalimbali za afya, kufanya ukarabati wa vituo 159 vya kutolea huduma za afya na ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili ya utoaji wa huduma za afya ya mama na mtoto.
Sanjari na hilo Mhe. Othman amesema mpango utaimarisha mfumo wa magonjwa ya dharura na rufaa kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga pamoja na kuimarisha menejimenti na uwajibikaji katika utoaji wa huduma za afya na kwa upande wa Zanzibar mpango utaimarisha utoaji wa huduma za afya ya mama na mtoto pamoja na kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.
OR-TAMISEMI
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.