Na. Elinipa Lupembe.
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arumeru Magharibi Saad Mtambule amemkabidhi fomu za Uteuzi wa Ubunge Jimbo la Arumeru Magharibi ,Bw. Noah Lembris Mollel kupitia chama cha Mapinduzi -CCM
Mteule huyo wa Chama cha Mapinduzi, aliwasili majira ya saa 05:20 asubuhi, kwenye Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo, na kukabidhiwa fomu hizo za Uteuzi mnamo saa 05:53 asubuhi, akiwa ni mteule wa chama chama cha Mapinduzi kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo hilo.
Mgombea huyo aliwasili kwenye ofisi za Msimamizi wa uchaguzi, akiwa ameambatana viongozi wa chama hicho ngazi wilaya na kata, akiwepo, Katibu wa Chama wilaya ya Arumeru, katibu mwenezi wilaya, wajumbe wengine wa chama hicho pamoja na baadhi ya wateule wa Udiwani wa chama hicho.
Aidha Msimamizi huyo wa Uchaguzi, alimkabidhi fomu ya Uteuzi mgombea huyo, kufuatia Maelekezo ya Fomuya Uteuzi Na. 8B, kwa mujibu wa Kifungu cha 38 (3) na (4) chaSheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343 ikiweka wazi mambo yaliyojumuishwa kwenye fomu ya Uteuzi.
Msimamizi Mtambule amemtaka mteule huyo, kusoma maelekezo yaliyotolewa na Tume ya Taifa Ya Uchaguzi, kuheshimu na kufuata taratibu za Uchaguzi kwa kusoma vitini vyenye maelekezo ya taratibu zote za uchaguzi mkuu.
Aidha amemtaka na kufuata kanuni na taratibu za uchaguzi wakati wote wa kampeni, kwa kufanya kampeni za kistaarabu, ikiwa ni pamoja na kuepuka lugha za kashfa kwa wagombea wengine, lengo likiwa ni kufanikisha uchaguzi kwa amani, huru na haki kwa maendeleo ya wananchi wa Tanzania.
Mgombea huyo wa CCM, amefikisha idadi ya Wagombea kumi na mbilo, kutoka vyama kumi na mbili vya siasa, kuchukua fomu ya Uteuzi, Ubunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.