Na Elinipa Lupembe
Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Mhe. Costantine Simba, amekutana na waheshimiwa Madiwani na Wakuuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri ya Arusha, waliofika Jijini hapo kwa ajili ya ziara ya mafunzo Jijini hapo.
Akizungumza kwenye ukumbi wa mikutano wa Jiji la Mwanza, Mstahiki Meya, amewakaribisha wageni huku akiwathibitishia kuwa ziara hiyo ya mafunzo itakuwa yenye tija na kuzaa matunda kwa halmashauri zote mbili kwa maendeleo ya Taifa la Tanzania.
Mstahiki Meya amebainisha kuwa anayo matumaini makubwa kuwa, ziara hiyo itakuwa ya mafanikio kwa madiwani na watalamu kwa mustakabali wa maendeleo ya wananchi wa Halmashauri ya Arusha lakini pia ni njia sahihi ya kufungua milango ya kiuchumi na kijamii kati ya halmashauri hizo mbili za Mwanza na Arusha DC.
Amefafanua kuwa Jiji la Mwanza ni miongoni mwa Majiji yanakua kwa kasi huku wananchi wake wakijikita kwenye shughuli za biashara zaidi pamoja na uzalishaji wa kilimo na ufugaji kwa kiasi kidogo, huku shughuli hizo za kiuchumi na kijamii zikiwa ndio mategemeo ya mapato ya ndani ya Jiji la Mwanza.
"Wananchi wa Jiji la Mwanza kwa sasa wamejikita zaidi kwenye biashara kutokana na kukua kwa Jiji na kujikuta shughuli nyingine za kilimo na ufugaji zikiendelea kutokomea taratibu". Amesisitiza Mtahiki Meya huyo.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.