• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA MTAKUWWA ARUSHA DC YAIOMBA SERIKALI KUPITIA UPYA UKINZANI WA SHERIA DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: February 17th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Wajumbe wa Kamati ya Kupambana na ukatili wa kijinsia - MTAKUWWA halmashauri ya Arusha, wameiomba serikali, kuangalia namna ya kutekeleza sheria za kuwabana watu wanafanya ukatili kwa wanawake na watoto, kutokana na ukweli kwamba, jamii imeanza kubadilika na kutoa taarifa za matukio ya ukatili, lakini bado kesi zikikwama kutokana na baadhi ya sheria kukinzana.

Wajumbe hao, wameyasema hayo, wakati wa  kikao  kazi cha  'MTAKUWWA' cha kujadili taarifa za robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2021/2022, halmashauri ya Arusha, kilichofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa shirika la SOS- Children Ngaramtoni.

Akiwasilisha taarifa za shughuli za utekelezaji za MTAKUWWA, halmashauri ya Arusha kwa kipindi cha robo ya pili, Afisa Maendeleo ya Jamii anayesimamia Dawati la Jinsia, Lovil Nguyaine, amesema kuwa, licha ya kuwa bado changamoto ya ukatili wa kijinsia inaendelea kwenye jamii, kwa sasa jamii imeanza kupata ufahau kwa kutoa taarifa za matukio hayo kwenye sehemu husika ikiwa ni pamoja na polisi na baadhi ya kesi kufikishwa mahakamani.

Aidha Nguyaine ameweka wazi kuwa, katika kipindi cha kuanzia mwezi mwezi Oktoba mpaka Desemba,  jumla ya matukio  163 ya ukatili yameripotiwa na kufanyiwa kazi kupitia mamlaka mbalimbali za kisheria,  huku matukio 6 yakiwa polisi na mengine yako Mahakamani kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji.Hata hivyo, Afisa Jinsia huyo amethibitisha kuongezeka kwa matukio ya kutelekeza familia hata kufikia matukio 49 kwa kipindi cha miezi 3, hali ambayo inatishia maslahi na makuzi ya watoto, hivyo ni vema jamii ikaanza kuchukua tahadhari na sheria kuchukua mkondo pale mzazi atakapotelekeza familia.

Hata hivyo wajumbe hao, licha ya kukubaliana kuendelea kutoa elimu ya ukatilia kwa jamii, ili jamii iendelee kutoa ushirikiano hasa matukio hayo yanapofika kwenye vyombo vya usalama, polisi na mahakamani, lakini bado wameendelea kuzilalamikia sheria kinzani, zinazompa haki  mtuhumiwa wa ukatili na kusababisha wanajamii kukata tamaa na kushindwa kuendelea na kesi.

Wameongeza kuwa, endapo watuhumiwa wanaofanya vitendo vya ukatili na kuripotiwa kituo cha polisi na kufikishwa mahakamani, kesi hizo zikishughulikiwa kwa haki na kuwatia hatiani watuhumiwa hao, itasaidia kutokomeza ukatili dhidi ya watoto na wanawake katika jamii zetu.

"Inakatisha tamaa sana, mtoto amefanyiwa vitendo vya ukatili, amebakwa na mtoto anakiri kubakwa na kumtaja aliyemfanyia hivyo, lakini sheria bado inamlinda mbakaji, na wakati mwingine kumuachia huru, kwa vigezo ushahidi unaonesha hana hatia, hali hii inarusdisha nyuma harakati za kutokomeza ukatili kwenye jamii zetu" Wamesema wajumbe hao.

Awali Kamati ya Mkakati wa Taifa wa Kudhibiti Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto MTAKUWWA, halmashauri ya Arusha, kwa kushirikiana na wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali, inaendelea kutekeleza wajibu wake, kwa kupamba na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto huku mafanikio ya kamati hiyo yakiendela kuzaa matunda ndani ya jamii.

ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍✍









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.