• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MWEKEZAJI WA SHAMBA LA KORFAVOUN ESTATE Ltd ATOA EKARI 222 KWA KIJIJI NA WANANCHI WA LOSINONI KATI...

Posted on: September 30th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Hatimaye mgogoro uliodumu kwa muda mrefu kati ya wananchi wa kijiji cha Losinoni Kati kata ya Oldonyowas na mwekezaji wa shamba la Korfovoun Estate Ltd, umefikia kikomo baada ya mwekezaji huyo kuridhia kutoa sehemu ya shamba lake ekari 222 kati ya Eka 700 na kuwakabidhi wananchi wa kijiji hicho.


Mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya miaka 20, umefikia muafaka kwa mazungumzo na maridhiano baina ya mwekezaji na viongozi wa kijiji  yaliyoongozwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuella Mtatifikolo Kaganda na Kamati ya Usalama wilaya.


Akizungumza wakati wa kuoneshana mipaka ya maeneo hayo, mmiliki wa shamba hilo Bw. Robert Daniel, amesema kuwa amekabidhi eneo la Eka 222,  kwa kuzichanganua Eka 116 kwa serikali ya kijiji, Eka 23 kwa shule ya msingi Engedeko, Eka 11 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari na Eka 71 kwa wananchi ambao tayari walivamia na kujenga makazi yao.


"Eneo la shamba lililobaki tunatarajia kuanza kilimo cha pareto na mazao mengine hivyo ninaomba wananchi kushirikiana nami, katika shughuli hizo, kampuni itatoa ajira kwa wazawa wakati wote wa kutekeleza mradi wetu" Amesema Robert


Naye Mkuu wa wilaya ya Arumeru, mara baada ya kuoneshwa mipaka ya maeneo hayo, amemuagiza mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi kupitia Idara ya Ardhi, kuanza mchakato wa kuandaa kutenganisha hati ya shamba la mwekezaji na maeneo aliyoyatoa, kuweka mipaka maeneo yote yaliyotolewa kwa Umma, taasisi pamoja na kuwasaidia wananchi kurasimisha na kupima maeneo yao ili wapate hati miliki.


"Leo tumeoneshwa mipaka ya maeneo aliyoyatoa mwekezaji kwa kijiji, shule  na wananchi ambao tayari mlijenga kwenye shamba lake, ninakuagiza Mkurugeni na Idara ya Ardhi, zoezi hili lisichukue muda mrefu, maeneo yaliyotolewa kwa shule yawekewe 'bicon' na kuyapima,  wananchi wasaidieni kurasimisha na kuyapima waweze kupata hati miliki, ili mgogoro huu usijirudie tena" Amesema Mhe. Emmanuella.


Hata hivyo amewaagiza viongozi wa kijiji na vitongoji kuwaelimisha wananchi wao juu ya umiliki halali wa mwekezaji wa shamba hilo pamoja na kuheshimu mipaka ya shamba lake, kwa kuzingatia kuwa mwekezaji amewagawia maeneo kutoka sehemu ya shamba lake bure na zaidi hata wananchi waliovamia na kujenga ndani ya shamba ameridhia kuwaachia na kuruhusu wapimiwe na kumilikishwa kisheria.


Aidha amewasisitiza viongozi hao, kutoa ushirikiano kwa watalamu wa ardhi wakati wote watakapofika kijijini hapo kupima na kuweka mipaka maeneo hayo ili kurahisisha zoezi hilo liende kwa haraka na kukamilika kwa wakati.


Hata hivyo wananchi wa kijiji cha Losinoni kati wameishukuru serikali kwa kusimamia na utatuzi wa mgogoro huo wa muda mrefu ambao wamekiri ulikwamisha shughuli nyingi na kuchelewesha maendeleo yao.


Mwenyekiti wa Kijiji cha Losinoni Kati Mhe. Peter Gabriel amemshukuru Mkuu wa wilaya na  mwekezaji kwa kukubali kutoa sehemu ya eneo la shamba lake na kuwagawia wananchi na kijiji pia.


Ametupa eneo la shule ya msingi Eka 22, Eka 11 kwa ajili ya kujenga shule ya sekondari, lakini pia amerasimisha Eka 71 ambazo wananchi walivamia na kujenga, na Eka 116 kwa ajili ya kijiji chetu, tunamshukuru sana na nitawasimamia wananchi kumpa ushirikiano katika shughuli zake kilimo anazotarajia kuzifanya kijijini hapa" Amebainisha Mwenyekiti.


PICHA ZA MATUKIO








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.