Na Elinipa Lupembe
Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mhe. Ojung'u Salekwa akipanda mti kwenye eneo lililosimikwa mtambo wa kuchujia maji kijiji cha Lemanda.
Mhe. ojung'u ameotesha mti huo ikiwa ni ishara ya utunzaji wa mazingira muda mfupi kabla ya Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Balozi Yashushi Misawa, kuzindua mtambo wa kichujia maji na kuondoa madili ya floraidi.
Mtambo huo wa kuchujia maji umefanyika kwa ushirikiano mkubwa wa Serikali ya Japan kupitia chuo kikuu cha Shinshu na serikali ya Tanzania ili kuondoa taka hususani madini hatari ya floride madini ambayo yamekuwa ni changamoto kwa afya za wakazi wa kijiji cha Lemanda.
Mtambo huo wa kuchuja maji wenye uwezo wa kuzalisha Lita 300 kwa saa na kuhudumia jumla ya 60 na watu zaidi ya 400 wa kitongoji cha Lemanda na umegharimu dola za kimarekani 115,000 sawa na shilingi milioni 264 za kitanzania.
Mtambo huo wenye uwezo wa kuchuja na kuondoa madini ya floraidi kutoa mm 24 kwa lita na kufikia mm 0.1 kiwango ambacho kinakubalika kwa mataifa, maji ambayo yatatumiwa na wananchi hao kwa ajili ya kunywa na kupikia.
Wananchi wa Lemanda wameushukuru ubalozi wa Japani kwa msaada huo, ambao wanaamini utakwenda kupunguza madhara wanayoyapata kutokana matumizi ya maji yenye kiasi kikubwa cha madini ya floraidi.
ARUSHA DC Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
#KaziInaendelea✍✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.